MCHOME AMKALIA KOONI LISSU AMTAKA AKUBALI KUKOSOLEWA
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro Lembus Mchome ambaye pia ni miongoni mwa wafuasi wa G55 amemtaka Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Tundu Lissu kukubali kukosolewa na wanachama ili kusimamia na kuiheshimu demokrasia anayoihubiri muda wote.
Mchome ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam mapema leo Aprili 8,2025 wakati akizugumza na waandishi wa habari ambapo amesema siasa safi ni lazima mtu akubali kukosolewa na kupokea mawazo mbadala.
Amesema baadhi ya Viongozi wa chama wamekuwa hawakubali kukosolewa, akiwemo Mwenyekiti wa Taifa Tundu Lissu licha ya kuwa muumini wa demokrasia hiyo
"Katika mikutano amekuwa anasema kuna wajinga wajinga wanahoji... mwenyekiti wa chama unawaita wanachama wajinga jinga,hutaki kukosolewa umekuwa Mungu hutaki kusikiliza hoja mbadala kwa nini badala usikilize tukubali kukosolewa,naomba mwenyekiti wangu ukubali kukosolewa ili tuweze kujenge Chadema imara yenye nguvu,”alisisitiza Mchome.
Aidha Mchome amemuomba Msajili wa Vyama Vya Siasa kubatilisha maamuzi ya Baraza Kuu la Chadema lililofanyika Januari 22 mwaka huu.
Amesema katika kikao cha Baraza Kuu ambalo pia kilimthibitisha Katibu Mkuu John Mnyika pamoja na viongozi wengine wakuu saba si halali kwakuwa akidi ya wajumbe wa kikako hicho haikuwa imetimia kama inavyoelekezwa katika katiba ya chama.
"Kiutaratibu ili kikao kianze ni lazima mwenyekiti awe na orodha lakini katika kikao kile katibu mkuu anakiri ni kweli hawana akidi kwakuwa hawakuwa na orodha na kama alikuwa nayo basi aipeleke kwa Msajili wa Vyama vya Siasa ili aihakiki"amesema
Pia amemuomba msajili kubatilisha maamuzi yote yaliyofanywa Januari 22 kwakuwa hayakuwa na uhalali kulingana na aina ya wajumbe waliyoyapitisha.
Post a Comment