Ads

TMA YAWAJENGEA UWEZO WANAHABARI KURIPOTI TAARIFA KWA USAHIHI

Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a akifungua  Warsha  kwa waandishi wa habari kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu muelekeo wa msimu wa mvua za masika kuanzia mwezi machi hadi mei Mwaka huu, warsha hiyo imefanyika leo tarehe 21/2/ 2023 Kibaha, Mkoani Pwani.


Waandishi wa habari wakiwa katika majadiliano kuhusu namna ya kuripoti taarifa za hali ya hewa kwa usahihi.

Mkuu wa kitengo Cha Mawasiliano Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Bi. Monica Mutoni akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika warsha iliyofanyika leo tarehe 21/2/2023 Kibaha, Mkoani Pwani.

 Na Noel Rukanuga, Pwani

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imewataka waandishi wa habari kuendelea kufatilia na kuripoti taarifa za hali ya hewa kwa usahihi jambo ambalo litasaidia kupiga hatua katika nyanja mbalimbali za kimaendelea.

Akizungumza leo tarehe 21/2/2023 Kibaha, Mkoani Pwani wakati akifungua warsha ya waandishi wa habari kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu muelekeo wa msimu wa mvua za masika kuanzia mwezi machi hadi Mei Mwaka huu, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Ladislaus Chang’a, amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia wanahabari katika kufanya kazi zao kwa ufanisi.

“Warsha hii ni muendelezo wa juhudi za kuhakikisha taarifa mbalimbali zinawafikia jamii kwa usahihi ili kuleta tija na kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kwa kutoa taarifa ambazo sio sahihi” amesema Dkt. Chang’a.

Dkt. Chang’a amewataka waandishi wa habari kuendelea kuwa Mabalozi wazuri kwa umma, huku akitoa wito kwa jamii  kuendelea kufatilia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ili waweze kupata uelewa mpana.

Amefafanua kuwa katika kipindi hiki Mamlaka imekuwa ikifanya utabiri katika maeneo madogo madogo kuanzia ngazi Wilaya hasa yanayopata msimu mmoja wa mvua.

“Mnafanya kazi kubwa muhimu katika jamii, hivyo tunaomba iendelee kwa  kutoa elimu na kutambua Mamlaka ya Hali ya Hewa ndiyo yenye dhamana ya kutoa taarifa zote zinazohusiana na Hali ya Hewa” amesema Dkt Chang’a

No comments