Ads

WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI KUONGEZA NGUVU MABORESHA UTENDAJII WA TAZARA.

 

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Atupele Mwakibete akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya watendaji wa Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) wakiwa katika kikao kazi na Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Atupele Mwakibete.

.......

Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imesema itatatua changamoto mbalimbali zilizopo katika Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) ili kuendelea kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam wakati alipofanya ziara Shirika la TAZARA Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Atupele Mwakibete, amesema Wizara yake itaunda Bodi Maalumu ambayo itakua inashughulikia changamoto za TAZARA.

Amesema kuwa serikali ya Tanzania na Zambia zimeanza kufanya mchakato wa kubadilisha sheria ili kufanya marekebisho, kwani sheria iliyopo kwa sasa inazuia kufanya uwekezaji wowote upande wa Tanzania bila kukubaliana na serikali ya zambia.

 “Tunashindwa hata kuendeleza upande wetu wa serikali kwa sababu sheria iliyopo inazuia kuwekeza chochote katika reli hii mpaka tukubaliane na wenzetu, hivyo tayari mchakato wa kubadilisha sheria hii unaendelea tukikamilisha hata baadhi ya changamoto zitapungua ”amesema Naibu Waziri Mhe. Mwakibete.

Naibu Waziri Mwakibete amesema kuwa shirika hilo linakumbwa na changamoto malimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu , madeni makubwa ya wafanyakazi hali ambayo inachangia shirika kushindwa kujiendesha kwa ufanisi mkubwa.

Amesema kuwa kuwa baadhi ya wafanyakazi wa TAZARA hawapewi mikataba ya kudumu ya ajira hali ambayo inawafanya wakose morali ya kufanya kazi, huku akisema kuwa suala hilo linafanyiwa kazi na serikali.

Meneja Mkuu wa TAZARA Tanzania Fuad Abdallah, amesema kuwa TAZARA inakumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu, upungufu wa mabehewa na injini ,madeni ya wafanyakazi, madeni ya mifuko ya kijamii pamoja na madeni ya wasanbazaji .

No comments