Ads

Imamu Mkuu Msikiti wa Tambaza ahitimisha dua ya Rais

 Na Dunstan Mhilu, Dar es Salaam.

IMAMU Mkuu wa Msikiti wa Tambaza na Shehe wa Kata ya Upanga Magharibi Athuman Mohamed amehitimisha dua ya kumuombea Rais Samia Suluhu Hassan iliyodumu kwa siku saba.

Dua hiyo ilianza siku Rais alipotimiza miaka 62, kama siku ya kumbukizi yake ya kuzaliwa na hivyo wanafunzi wa Madrasa ya Tambaza walimuomba Imamu huyo kufanya dua maalumu yakumuombea Rais.

“Tunamshukuru Mungu tumehitimisha dua maalumu ya kumuombea Rais wetu mpendwa tuliyoendesha na wanafunzi wa madrasa kwa malango saba, katika kanuni zetu tunawaombea viongozi wote kila siku ila hii ilikuwa maalumu kwake kwakutimiza miaka 62 yakuzaliwa kwake”alisema

Ameongeza kuwa maombi na dua dhidi ya viongozi ni endelevu kikubwa wanaomba utulivu na amani uliopo nchini uendelee kwani Mungu humpendeza zaidi kutuona tukiwa na amani na furaha tele lakini Rais pia hutekeleza majukumu yake kikamilifu kukiwepo na amani.



Akiendesha Ibada hiyo iliyokuwa rasmi kwa wanafuzi wa madrasa kumtakia heri Rais Samia alisema ni ombi na ombwe la wanafunzi wa Madrasa ya Msikiti wa Tambaza kuomba kumfanyia dua Rais.

“Ndugu waandishi wa Habari leo hii  tunahitimisha dua maalumu tunawashukuru kushiriki pamoja nasi katika dua maalumu ya kumuombea Rais wetu ili Mwenyezi Mungu kupitia Mtume (SAW) ampe heri na Afya njema ili atimize kusudi la kiimani kuongoza nchi na wananchi wake”alisema

Aidha Imamu huyo alisema kutimiza miaka 62 si jambo dogo ni umri mkubwa hivyo kutokana na umuhimu wake kwa Taifa lazima viongozi wa dini wamfanyie du ana kumuombea kila wakati ili afanye kazi zake kwa uhuru na umakini zaidi.

“Dua hizi na maombezi huondoa dhoruba na sisi viongozi wa dini tumepewa jukumu lakuombea nchi,Viongozi wa juu akiwemo Rais wake,wasaidizi wake na wote wenye mamlaka hivyo tunatimiza takwa la kiimani” alisema

Kwa upande wao Wanafunzi wa Madrasa hiyo walipata nafasi yakuzungumza baada ya Dua hiyo walisema kuwa wanawapenda viongozi wote wa nchi na huwaombea kila siku ispokuwa juzi ilikuwa ni siku maalumu kwa Rais kwasababu ni siku muhimu ya Rais.

“Sisi wajukuu zake wa Madrasa ya Tambaza tunampongeza Rais kwakutimiza siku yake yakuzaliwa japo tumempongeza leo wenzetu mbalimbali walimpongeza siku yake yakuzaliwa na sisi tunamfanyia dua leo tunaamini hatujachelewa baada ya kumuomba Imamu wetu Shehe Athuman na kutukubalia basi tunamuombe Maisha marefu kwa Mola afanye kazi bila wasiwasi tunamuombea”alisema mmoja alisema Samira Mwanga

Naye Najash Sillia mwanafunzi wa Madrasa hiyo alisema wanaguswa na jinsi Rais anavyosimamia haki za Watoto ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa ambapo weanafunzi wote wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza wameanza masomo bila shida.

“Rais amewasaidia wazazi wetu kwakugharamia ujenzi wa vyumba vya madarasa na utengenezaji wa madawati kwani kila mwaka Januari wazazi walikuwa wakichangishwa hela za madawati lakini sasa ndugu zetu wote waliopaswa kuanza la kwanza na kidato cha kwanza wameanza bila shida.

No comments