Ads

MRATIBU WA THRDC ANENA MAZITO WAJIBU WA SERIKALI KULINDA HAKI ZA BINADAMU.

Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Onesmo Olengurumwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
.......................

Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) Onesmo Olengurumwa amesema kwa mujibu wa katiba na sheria za kimataifa mwenye jukumu la kulinda haki za binadamu ni serikali pamoja na taasisi zake zikiwemo mahakama pamoja na jeshi la polisi.

 Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu

Tanzania (THRDC) Bw. Onesmo Olengurumwa amesema kuwa ni vyema haki za binadamu zikaendelea kuheshimiwa ili ziweze kusaidia kuitetea jamii katika changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo.

 "Tunafahamu kwamba ulinzi wa haki za binadamu mwenye jukumu la kwanza la kulinda haki hizo kwa mujibu wa katiba na sheria za kimataifa ni serikali zetu na taasisi zake na ndio maana tuna polisi,"amesema Olengurumwa .

 Imeeleza kuwa Taasisi za haki za Binadamu zikizingatia misingi ya kikatiba na kisheria na haki za binadamu zitasaidia kulinda haki hizo na kuondoa changamoto kwa jamii.

 Amesema ni vyema haki za binadamu zikaendelea kuheshimiwa ili ziweze kusaidia kuitetea jamii katika changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo.

 Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu Mohamed Hamis Hamad amesema ili kuzilinda haki za binadamu ni vyema taasisi za kiserikali zikatumia nafasi zao katika kuzisimamia taasisi.

 "Ukizungumza Haki za binadamu unazungumza kuishi katika mazingira mazuri, afya,kuishi, chakula hivyo ukikivunja kimoja kinakuplekea katika mazingira mengine kwa hivyo kwa misingi hiyo kuna haja ya kuimarisha juhudi za pamoja baina ya serikali na wadau wote wa haki za binadamu,"amesema Mohamed

 Mkutano na mafunzo ya siku tatu inayohusisha Mtandao wa Taasisi za haki za Binadamu Afrika wakijadili la Marakeshi ambalo limeweka utaratibu mzuri wa kulinda haki za binadamu.

No comments