Ads

Mwlekeo mpya faini za barabarani



 Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelitaka jeshi la  Polisi kutotumia makosa kama kitega uchumi kwa kutoza faini Madereva  badala yake lijikite zaidi katika  kutoa elimu.

Rais Samia Ameyasema hayo katika hafla ya Kuzindua Kiwanda cha Ushonaji sare za polisi kilichopo Bohari Kuu ya  Polisi Kurasini Jijini Dar es salaam.


Aidha  Rais Samia ameyataka majeshi mengine kuiga mfano wa  jeshi hilo kwa kushona sare zao katika kiwanda hicho na kwamba  hatua hiyo  itadhibiti uingizwaji wa sare bandia mitaani  na kuokoa fedha za  serikali.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo, mkuu wa jeshi la polisi  nchini Simon Sirro, amesema takribani bilioni 50.1  zimekusanywa na polisi kutokana na makosa ya tozo za usalama barabarani kati ya Julai 2020 hadi Aprili 2021 wakati shilingi bilioni 56 zilizokusanywa kati ya Julai 2019 hadi Julai 2020.


No comments