Ads

IGP Simon Sirro leo amemuapisha kamishina msaidizi wa Polisi ACP Salum Hamduni kuwa Kamishna

 


Mkuu wa Jeshi la  Polisi nchini  Simon  Sirro  leo amemuapisha kamishina msaidizi wa Polisi ACP Salum  Hamduni kuwa Kamishna wa Polisi,  jijini Dar es salaam.

kiapo hicho kimekuja baada ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe,  Samia Suluhu Hassan kumteua   kuwa Kamishna na Mkurugenzi wa Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa   TAKUKURU.

IGP Sirro amempongeza kamishina  HamdunI kwa weledi aliouonyesha katika utumishi wake ndani ya Jeshi la Polisi hasa alipokuwa Kamanda wa Polisi katika mikoa ya Ilala, Njombe, Kilimanjaro, Arusha na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum Dar es salaam.

Kwa upande wake  Kamishina - SALUM  HAMDUN amemshukuru Mhe, Rais Samia Suruhu kwa kumuamini katika nafasi hiyo huku akilishukuru Jeshi la Polisi kwa nafasi alizopata na kuzifanyia kazi kwa weledi mkubwa.

No comments