Ads

JAMII FORUMS NA CDF ZAINGIA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO KIKAZI ,KUTOA ELIMU ,KUPINGA UKATILI



Mkurugenzi mtendaji wa CDF  Koshuma Mtengeti  aliye upande wa kushoto na aliye upande wa kulia ni Mkurugenzi  wa Jamii forums Maxence Melo  wakionesha mkataba wa makubaliano  ya ushirikiano walio usaini baina  ya taasisi zao  leo jijini Dar es salaam.( Picha na John Luhende)

Mkurugenzi mtendaji wa CDF  Koshuma Mtengeti  aliye katkati  na aliye upande wa kulia ni Mkurugenzi  wa Jamii forums Maxence Melo  wakisain  mkataba wa makubaliano  ya ushirikiano  baina  ya taasisi zao  leo jijini Dar es salaam.( Picha na John Luhende)

 Na John Luhende 

Jukwaa la Utu wa Mtoto (CDF) na. asasi ya  kiraia ya Jamii Forums ambayo inaratibu mtandao maarufu nchini wa Jamii Forums leo wamezindua ushirikiano  wa kikazi.

Akizungumza Katika uzinduzi huo  Mkurugenzi mtendaji wa  CDF  Koshuma Mtengeti , amesema ushirikiano huo unalengo la kukuza uelewa wa haki na ustawi wa Mtoto wa kitanzania Katika harakati za kutokomeza  ukatili dhidi ya Watoto ikiwemo  mimba za utotoni , ukeketaji, ndoa za utotoni,ubakaji na ulawiti ,vipigo, matusi matusi na udhalilishaji wa utu wa mtoto.

Amesema Katika ushirikiano huo  utawezesha  kutoa elimu kupitia mtandao wa Jamii Forums ambao unaongoza kwa kusomwa na watu wengi ndani na nje ya nchi ukiwa na wasomamaji takribani  Milioni  kumi Kila mwezi   jambo ambalo litawezesha kutoa elimu kwa jamii juu ya Sheria na Sera zinazo mlinda mtoto wa kitanzania, mila na tamaduni zinazo zinazomkandamiza mtoto, wajibu wajamii  kwa mtoto .

Aidha elimu itatolewa  juu ya namna ya kuripoti kesi za ukatili katika vituo husika  moja wapo ikiwa no katika dawati la jinsia na watoto, vituo vya mkono kwa mkono ili kuwezesha kupatikana kwa haki.

Ushirikiano pia utasaidia kupaza sauti na kutoa elimu kwa jamii na wahanga  wa matukio ya ukatili kujua haki zao  na kuendeleza juhudi zinazo fanywa na Serikali, Asasi za kiraia , wadau wa maendeleo, Vyombo vya habari.

Kwamujibu wa utafiti uliofanywa na taasisi yakuzuia na  kupambana na rushwa TAKUKURU  umeonesha kuwa asilimia 84.5% ya  vitendo vya  rushwa ya ngono  hufanyiwa wanawake na asilimia 15.4 hufanyiwa wanaume .

Utafiti mwingine wa Demographia na Afya   TDHS  za mwaka 2015/2016 unaonesha asilimia 36 ya wanawake nchini Tanzania wanaolewa kabla ya kufikia umri wa miaka 18.

Ripoti ya Haki za Binadamu  ya mwaka 2019 iliyo tolewa na kituo Cha Sheria na haki za Binadamu  ilibainisha  asilimia 84 ya  matukio ya ukatili dhidi ya Watoto yaliripotiwa na vyombo vya habari mwaka 2019 ni ya ukatili wa kingono, pia matukio 42,824 ya ukatili wa kijinsia  dhidi ya Watoto  yaliripotiwa Polisi mwaka 2016-2019  yalikuwa ya ukatili wa kimwili,kingono, utumikishwaji kazi,ubaguzi kwa wanaoishi na ulemavu.

Utafiti mwingine wakidemographia na Afya TDHS wa mwaka 2015-2016 unaonesha asilimia 27%ya wasichana Kati ya miaka 19 walipata ujauzito .

 Kwa mwaka 2003 -2011 wanafunzi 55,000 waliacha shule  kwa sababu ya mimba za utotoni  wengi wakiwa kati ya miaka 13 hadi 18.

No comments