Ads

UTEUZI WA MKURUGENZI WA MAMLAKA YA MAJISAFI NA USAFI WA MAZINGIRA – MOROGORO


Waziri wa Maji Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb) amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi  na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA).

Taarifa ya Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo imemtaja aliyeteuliwa kuwa ni Mhandisi Tamimu Twaha Katakweba. Aidha, kufuatia uteuzi huu Mhandisi Katakweba anakuwa Katibu wa Bodi ya Wakurugenzi wa MORUWASA.

Uteuzi huu umefanyika chini ya Sheria Namba 5 ya Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019.

No comments