Ads

Meya Kumbilamoto atoa neno zito kwa walemavu.



Na John Luhende 
Mwambawahabari 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto, ameitaka jamii kuwaungamkono watu wenye ulemavu katika kazi zao ilikuwasaidia kujikimu kimaisha na kuacha utegemezi kwa kuomba omba mitaani.
Meya Kumbilamoto ametoa kauli hiyo alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa album ya nyimbo  za injili inayo julikana kwa jina la Kalipia gharama zote , ya mwimbaji Steven Mkami ambaye ni kipofu,  huku akimtaka  mwimbaji huyo kutokata tamaa  ya maisha  serikali imeweka utaratibu wa kuwasaidia walemavu.
“Naomba wadau wa maendeleo waweze kumsaidia huyu kijana ameamua kutumia kipaji chake kumwimbia Mungu angeweza hata kuimba nyimbo za kidunia ( Bongoflava ) lakini ameona kunamaisha baada yamaisha haya nay eye anatafuta Paradiso“Alisema 
Kumbilamoto kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya ya Ilala mhe.Sophia Mjema  wameweza kumsaidia mwimbaji huyu jumla ya shilingi 500,000 ambapo ametumia fursa hiyo kuwahimiza walemavu kujiunga katika  vikundi ili  waweze kufaidika na mikopo inayotolewa na Manispaa badala ya kubaki wakiomba omba mitaani.
“Tunamshukuru Rais John Pombe Magufuli kwa kuweka mikopo ya asilimia mbili kwa walemavu sasa wanaweza  kukopeshwa na kufanya kazi zao kwa uhuru  na omba nitoe wito kwa walemavu wote ,waige mfano wa Steven Mkami angeweza kuchukua kopo na kwenda mnazi mmoja kuomba lakini akaamua kutumia kipaji chake “Alisema Kumbilamoto.
Kwa upande wake Steve Mkami  amewaomba watu wote wenye mapenzi mema kumsaidia ili awe na makazi aweze kufanya kazi zake uimbaji  kwa uhakika kuliko hivi sasa ambapo amesema anapanga.
“Mimi nilianza uimbaji mwaka  2012 nilianza uimbaji ,kwa wale ambao hawanifahamu mimi  nilizaliwa nilikuwa naona  lakini nilizidishiwa dawa ya kwinini  macho yakapata presha  hatimaye nikashindwa kuona ,ninachohitaji kwasasa  ni msaada kuhusu makazi nina familia na watoto nina yeyote atakaye guswa anaweza kunisaidia’’Alisema Mkami.
Aidha Mkami amewataka waimbaji wa nyimbo za injili kuwa na ushirikiano na kusema kuwa waimbaji hao wamekuwa hawana ushirikiano ukilinganisha na waimbaji wa nyimbo za kidunia ,huku akidai kuwa hata yeye alialika  baadhi ya waimbaji lakini wamekuwa wakitaka kupewa fedha  ilikushiriki naye katika uzinduzi.
Nao baadhi ya  waalikwa waliofika kuchangia uzinduzi huo  wamepongeza  hatua ya mwimbaji huyo na kumshukuru Mungu kwa kuwa amempa ujasili wam kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia kipaji chake .
“Tujifunze kwa Yesu mwemyewe alikuja kutusaidia sisi tukiwa wenye dhambi  kwahiyo tusijali kwamba labda huyuniadui yangu bali tuwatendee mambo mema ‘Alisema Donald  Mushi.

No comments