Ads

KUMBILAMOTO, ATOA UJUMBE MZITO KWA JAMII KUHUSU WAJANE NA WALEMAVU.



Na. John Luhende
Mwamba wa habari
Wajane na waleva waishio  kata ya Vingunguti  Manispaa ya Ilala , wametakiwa kuwa na umoja na ushirikiano ilikuweza  kufanya biashara ndogondogo zitakazo wasaidia kukidhi mahitaji yao ya kila siku na kumudo kurejesha  fedha za mikopo ambayo wanatarajiwa kukopeshwa na Manispaa.

Kauli hiyo imetolewa na Diwani wa Kata ya Vingunguti  ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa  ya Ilala Omary Kumbila moto wakati  wa mafunzo mafupi ya ujasilia mali  yaliyofanyika  chini ya Maafisa mikopo na Afisa vijana wa Manispaa ya  Ilala  , ambapo pia  amegawa Mikate 400, kwa makundi hayo.

Aidha kumbilamoto  ameitaka jamii   kuto yanyanyapaa  makundi  hayo kwakuwa kufanya hivyo ni  kinyume na agizo la  Mwenyezi Mungu.

“Makundi ya yatima wajane na walemavu alisisitiza sana Mwenyezi Mungu tuyatazama sana  kwa jicho la huruma na kuya saidia  hivyo nawaomba sana viongozi wenzangu  kwa hali na mali tujitolee misaada  , nashukuru pia kama manispaa tumetenga  takribani million 700 kwaajili ya mikopo “Alisema Kumbilamoto.

Mwamba wa habari  pia imezungumza na Makundi yote yaliyo hudhuria mafunzo hayo   ambapo Ester Toi  Nzigo, ambaye anatoka kundi la Mama wajane  amesema mikopo hiyo itawasaidi kwakuwa ninafuu kuliko hapa awali ambao mikopo hiyo ilikuwa inatolewa kwa Riba kubwa .

“Tuta mudu kulipa mikopo hii kwa kuwa tumesha zoea kulipa mikopo riba tutapata unafuu mkubwa  tuna mshukuru sana Diwani wetu Kumbilamoto ,Rais Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia, alituahidi kuwa wananawake tutapewa mikopo sasa yametimia “Alisema 

“Sisi walemavu  mikopo hii itawasaidia kuondokana na hali ya kuomba omba mitaani sasa tutakuwa na biashara zetu “Alisema Fides Mwakilema  .

No comments