Ads

RC MAKONDA AWANUSURU KUKOSA MASOMO WANAFUNZI 31,092 SAWA NA 47% YA WATOTO 64,861 WALIOFAULU.




Mwamba wa habari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Mhe. Paul Makonda amewahakikishia  wanafunzi 31,092 sawa na 47%  ya watoto 64,861  ambao walifaulu katika mkoa huo kuendelea na masomo yao ya  kidato cha kwanza  kwakuwa serikali imeanza  ujenzi na ukarabati wa vyumba vya  madarasa 622  ili kuhakikisha  hakuna mwanafunzi atakaeachwa  kwa kigezo cha  uhaba wa madarasa. 

RC Makonda  amesema  ongezeko la wanafunzi na ufaulu  ni matokeo ya mafanikio ya  Rais Dkt. Magufuli  kutenga fedha zaidi ya bilioni 29  kwaajili ya elimu Bure ambapo kati ya hizo  Bilioni 17.46  zinaenda kwenye  elimu ya sekondari na tayari  Serikali imejipanga  na kuhakikisha kuwa tangu  January 07 shule zote 147 za sekondari zimefunguliwa  hivyo  kila mzazi ahakikishe anamuandikisha mtoto  ili kuendelea na kidato cha Kwanza.

Aidha RC Makonda  amesema katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba mkoa huo umekuwa  kinara kwa kufaulisha wanafunzi 64,861 sawa na  92%  ambapo kati ya hao Wanafunzi 31,092  walikosa  vyumba vya madarasa  jambo lililoilazimu serikali kupambana kuhakikisha  kila aliefaulu anaendelea na masomo.
Hata hivyo  RC Makonda  amesema lengo la  ujenzi wa madarasa  hayo ni kuhakikisha kila mwanafunzi anatumia  fursa ya Elimu Bure iliyotolewa na Rais Dkt. John Magufuli  ya kuhakikisha  Mtoto wa maskini anasoma  ili kujikwamua  kiuchumi  na mwisho wa siku Taifa liwe na  wataalamu wa kutosha.


Katika hatua nyingine,Makonda amesema mpango wa Serikali ni kuhakikisha Mkoa huo unakua ni wa Usiku na Mchana hautazidi mwezi wa pili.

Makonda ameyasema hayo Leo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisi kwake na kusema kuwa zipo changamoto ambazo wamekuwa wanahangaika nazo kuzitatua ni pamoja na kuwa na taa za ulinzi kwenye maduka na kuwasihi wafanyabiashara wafunge kamera. na punde watakutana na wafanyabiashara wote.

"Mpango wa Serikali ya Mkoa ni kuhakikisha kwamba DSM inakua ni ya usiku na mchana, hautazidi mwezi wa pili kutakua na tamko rasmi la kuhakikisha DSM ni ya usiku na mchana" -RC Paul Makonda
 Pia amesema punde watakutana na wafanyabiashara wote ili kujadili swala hilo.

No comments