NAIBU WAZIRI STELLA IKUPA : WATOTO YATIMA NI WATOTO WETU TWAPATIENI MSAADA
Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu Stella Ikupa ,akimkabidhi Beatrice Laurence ,Afisa ustawi wa Jamii,Baadhi ya vitu alivyo toa msaada katika makao ya watoto yatima kurasini,aliye upande wa kushoto ni Mbunge wa viti maalumu Temeke, Mariam Kisangi.(Picha zote na John Luhende)
Na John Luhende
Watanzania wameaswa kujitoa kwa hali na mali katika
kuwasaidia watoto yatima wanaoishi katika vituovya kulelea watoto kwani wanayo
mahitaji kama walivyo wengine wanaoishi majumbani na familia zao, kwa kuwa
kufanya hivyo ni kuugusa moyo wa
Mungu moja kwa moja .
Hayo
yamesemwa na Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu Stella Ikupa , alipo
tembelea na kutoa msaada katika Makao ya Watoto yatima Kurasini
,ambapo ametoa rai kwa watanzani
kuendelea kujitoa wanapo pata nafasi kutembelea na kutoa misaada kwa watoto
hao.
“Hawa ni
watoto wetu tuendelee kujitoa tunakaamajumbani kwetu tunakula na kusaza
tunamwaga vyakula kumbe kuna mtoto ambaye amelala njaa kwa sababu hana mzazi wa
kumhudumia , kwahiyo nijambo jema
tukitumia kidogo tunachokipata kugawana na wengine,hata Maandiko matakatifu yanasema, Dini iliyonjema ni kuwaona yatima na wajane katika shida zao
na mtu anapofanya hivi anamgusa Mungu”Alisema
Aidha Mhe.
Ikupa ameushukuru uongozi ya Makao ya watoto hao kwa kuendelea kuwalea vizuri watoto hao na kuupongeza uongozi wa CCM
kutoka Umoja wa wanawake (UWT) ambao nao waliambatana naye katika kutoa msaada
huo pamoja na Mbunge wa viti maalumu Mariam Kisangi .
Kwa upande
wake Afisa ustawi aliyemwakilisha Kamishina
wa Ustawi wajamii ,Kutoka wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii jinsia wazee na watoto,katika hafla hiyo
Rehema Kombe ,amemshukuru mhe. Stella
Ikupa, kwa moyo wake wa upendo na kuona umuhimu wa kuwasaidia na kutoa huduma kwa yatima na kusema kuwa watoto hao ni watanzania na wanamahitaji wanayo yahitaji kama wengine
na kutoa wito kwa viongozi wengine
kuwa na moyo huo .
“Watoto hawa
wamekosa wazazi wanahitaji ada za shule ,mavazi , chakula ,malazi na mengine
yaliyo mahitaji ya kibinadamu , tunapokuwa tunasherehekea tunafurahi huko
majumbani tuwakumbuke nawatoto hawa ,niwaombe sana viongozi , mashirika
,taasisi na watanzania kwa ujumla tuwajali niwatoto wetu sote kutoa nimoyo
ukitoa kidogo ulicho nacho Mungu anakubariki” Alisema
Wakitoa neno
la shukrani watumishi na baadhi ya watoto, wameshukuru kwa kuwajali na kuwathamini pia wamesema
wataendelea kumuombe kwa Mungu Mhe.Ikupa
ili amuongezee palipo pungua na kumfungulia Baraka .
Mariam
Kisangi ambaye ni Mbunge viti Maalumu
Temeke , Mkoa wa Dar es salaam,akizungumza Makaoni hapo, amewapongeza na
kuwatiamoyo walezi na wafanyakazi wa kituo
hicho na kuwaambia kuwa kazi wanayofanya ni kazi ya wito nikama kazi ya
mungu na fungu lao kubwa liko kwa Mungu
,huku akipongeza serikali kwa maboresho ya kituo hicho kwani kipindi cha
nyuma hakikuwa hivyo.
“Nawaomba
watoto wetu mpendane na muwapende walezi wenu na walimu wenu ili muendelee na
masomo”Alisema
Post a Comment