Ads

MAMA MLEMAVU ALIYESAIDIWA BAJAJI NAIBU WAZIRI STELLAIKUPA, ANENA MAZITO .



Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu  Stella Ikupa, akikabidhi funguo za Bajaji kwa Mama Leonea Leonard, ambaye ni mlemavu wa miguu makabidhiano hayo yalifanyika Jijini Dar es salaam(Picha zote na John Luhende)


Na. John Luhende 
Mwamba wa Habari
Wito umetolewa kwa wadau binafsi ,Makampuni na Mashirika mbalimbali kuwasaidia watu wenyeulemavu ,ili kukidhi mahitaji yao ikiwemo kuwaendeleza katika shughuli na vipaji vyao.

Witohuo umetolewa na Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi ,Vijana,Ajira na wenyeulemavu  Stella Ikupa,alipokuwa akikabidhi Bajaji kwa Mama Leonea Leonard ambaye ni mlemavu wa miguu ,ambapo amesema Bajaji hiyo ameipata kwakushirikiana na mdau baada ya kumweleza kuhusu shida ya Mama huyo.

“Wahitaji wako wengi Tanzania ,unawezakumsaidia Mama leonia au unaweza kumsaidia mhitaji mwingine ,leo tumempatia Bajaji inaweza kumsaidia katika shughulizake lakini pia bado analo hitaji lakusaidiwa kurecord nyimbo zake  
  ,tunaomba mdau mwingine aweze kujitokeza amsaidie aweze kurecord ‘’Alisema

Kwaupande wake Mama Leonea  Leonard ,amemshukuru Mhe. Stella Ikupa,  kwa moyo wake wa kujali watu bila kujali kuwa ni ndugu yake ama kuwa anaulemavu bali anasaidia watu wote ,amesema watu wengi wanauwezo kifedha lakini  hawana moyo wa kusaidia ,Bajaji hii angeweza kuitumia kwa mambo yake  mengine lakini kaamuamua kumpatia yeye hivyo amemshukuru Mungu kwa Upendo huo.

‘’Stella Ikupa  ,Joshua  na Mkewake  kwapamoja nawashukuru sana Mungu awabariki ,Kwa nisaidia Bajaji hii sina cha kusema sana zaidi ya kuwashukuru na kuwaombea Mungu awainue mzidi kufanikiwa ,Bajaji hiimimi itanisaidia sana sina mahali pa kuishi naweza kukusanya kidokidogo nami niwe na makazi yangu  na pia nahitaji sana kurecord nyimbo zangu”Alisema.

Mama Leonia amesema yeye hakuzaliwa na ulemavu bali alipata ajali ya gari  miaka minane iliyopita ,ambapo katika ajali  hiyo walikufa watu kumi nakupona wawili akiwemo yeye,pia ameelezakuwa yeye ni fudi  kushona nguo  ila hana mashine na anakipaji cha kuimba nyimbo.











No comments