Ads

KITUO CHA UWEKEZAJI NCHINI (TIC) CHAFURAHISHWA NA HATUA YA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI, KWA KUWAPA WIZARA KAMILI.






Mkurugenzi wa kituo cha uwekezajiji  (TIC) Geofrey Mwambe, akizungumza na waandishi wahabari (hawapo pchani) pamoja na maafisa wa kituo hicho leo jijini Dar es slaam( Picha na John Luhende).





Mkurugenzi wa kituo cha uwekezajiji  (TIC) Geofrey Mwambe, akizungumza na waandishi wahabari pamoja na maafisa wa kituo hicho leo jijini Dar es slaam( Picha na John Luhende).


Na.John Luhende 
Mwamba wa habari
Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC, kimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DKT John  Magufuli  kwa kufanya maamuzi ya kuanzisha Wizara inayoshughulikia  masuala ya uwekezaji, tofauti na awali ambapo shughuli zote za TIC  zilikuwa chini ya Wizara ya Viwanda,Biashara  na Uwekezaji .

Akizungumza na waandishi  wa habari  jijini  Dar es Salaam, Mkurugenzi wa TIC,  Geofrey  Mwambe, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa. Dkt John Pombe Magufuli,  kwa kuona umuhimu wa kukihamishia Kituo  hicho ofisi ya Waziri Mkuu,  kwani kitarahisisha  utekeleji wa majukumuyake ikiwemo kusukuma haraka  juhudi za  uanzishwaji wa Viwanda nchini.

Ameongeza kuwa, TIC  ni muhimu kwa kujenga uchumi wanchi  na kwamba kitendo cha kituo hicho kupewa Waziri wake na Katibu  mkuu wake utaharakisha  na kurahisisha  utekelezaji wa mipango yake,hivi karibuni Rais Magufuli, alimteua Mhe. Angellah Kairuki, kuwa waziri wa Uwekezaji na Doroth Mwaluko, kuwa katibu mkuu.

Aidha ametoa wito  kwa taasisi binafsi, taasisi za Serikali  pamoja na  serikali za mitaa, kushirikiana na TIC  katika kutangaza fursa za uwekezaji ndani na nje ya nchi.

"Jana nimeongea sana na Waziri wa Fedha, amesisitiza tujitahidi sana kujenga mazingira ya uwekezaji na yawe rafiki zaidi asiwepo mtu wa kukwepa kulipa kodi na tukifanya hayo tutamsaidia sana Rais na wawekezaji waendelee kuiona Tanzania kuwa nchi salama katika Uwekezaji "Alisema Mwambe.

Hata  hivyo amezitaka taasisi binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali,   kushiriki kikamilifu katika kutangaza fursa za uwekezaji  na kusema kuwa hali ya uwekezaji Duniani mwaka 2018,  ilishuka kwa 23%  kwa Afrika Mashariki Tanzania  ilipata Dola za kimarekani  billion 1.365 mwakaka 2017,mwaka 2018 ilishuka hadi dola za kimarekani  billion 1.2  lakini iliongoza  Afrika Mashariki na kufanya vizuri kimataifa.

" Nimeona clip ya Tundu Lissu alipokuwa akihojiwa na kituo cha televisheni huko nje ya nchi, huo siyo uzalendo  inaonekana Mtangazaji  anajua zaidi anaipenda Tanzania kuliko yeye, nimemshangaa  sana ,anaibomoa nchi wakati yeye ndiyo anasema anataka kugombea 2020"alisema.

Watanzania wanalo jukumu kubwa kuisemea vizuri nchi yao kimataifa na kwamba inaongoza kuwa na mazingira Mazuri ya uwekezaji na haina tishio lolote la kigaidi kama iliyo kwa nchi nyingine.

"Naomba sana wanahabari  na watanzania wote tushirikiane na Tundu Lissu naye ni mtanzania namuomba aache kuichafua nchi maana mwisho wa siku atarejea hapanchini, namimi  nita ongea naye, anatakiwa kuwa balozi wa Uwekezaji huko aliko"  Alisema.

Pamoja na hayo Mwambe ameishukuru Serikali kwa kuiongezea watumishi wa TIC  na Mikoa iliyotenga maeneo ya Uwekezaji.

"Naishukuru Mikoa ambayo imetenga maeneo ya uwekezaji na kuyapima hiyo itatusaidia  kwa wawekezaji wapya" Alisema.

Akijibu swali kuhusu wawekezaji wa kubwa amesema, Mradi wa kiwanda cha Cement  hengya Tanga ni moja ya  miradi mikubwa na unaendelea vizuri, katika eneo la mtimbwani Mkinga, kitakuwa kinatengeneza Cement marambili ya kiwanda cha Dangote cha Mtwara, kitakuwa na bandari yake kwaajili ya usafirishaji mizigo.


No comments