Ads

SEMINA YA KUWAJENGEA UWEZO WADAU WA HAKI YA AFYA YA UZAZI YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM CHINI YA TGNP MTANDAO

TGNP Mtandao kwa kushirikiana na shirika la Afrika Kusini la (Gender Links) wamekutanisha wadau mbalimbali wanaofanya kazi katika eneo la Afya ya Uzazi lengo likiwa ni kujadili changamoto zinazoikabili sekta hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari mapema jana jijini Dar es salaam na Afisa Programu ya Harakati na Ujenzi wa Nguvu za Pamoja wa TGNP Bi. Anna Sangai alisema kuwa wameamua kufanya mkutano huo ikiwa ni miongoni mwa sehemu ya kuendelea kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Aliendelea kusema kuwa malengo mengine ni kujitathmini kwa kina walipotoka, walipo na wanapoelekea katika swala la ukatili wa kijinsia pamoja na kuangalia kama taifa linaendana na mikataba mbalimbali ya kimataifa na kikanda ambayo nchi yetu imekubali kuingia na kuitekeleza.

Aidha ameongeza kuwa watoto wengi wa kike wamekuwa wakipata changamoto mbalimbali katika shule nyingi ikiwemo mazingira wezeshi kama vyumba vya kujihifadhia, ukosefu wa maji na hata baadhi ya shule hazina milango ya vyoo hali inayompa ugumu mtoto huyo.

"Shule nyingi kwa sasa zimekua hazina mazingira rafiki kwa wananfunzi wa kike, hivyo kupelekea kukumbana na changamoto mbalimbali, lakini mkutano huu utaangalia makubalino  ya kikanda na kimataifa ambayo yamelenga kuwepo kwa haki ya kijinsia "amesema Anna.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taatisi ya Center Against Gender Violence  (CAGBV) Sophia Komba amesema haki ya afya ya uzazi na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia hasa katika afya ya uzazi bado ni changamoto  kubwa sana nchini Tanzania. 

Ameongeza  kuwa, mkutano huo utajadili namna gani ya kuweza kukabiliana na changamoto za afya ya uzazi na kuweza kutokomeza kabisa ukatili wa kijinsia  ili kuwepo kwa usawa na upatikanaji wa huduma ya afya ya uzazi.. 

Aidha ameiomba Serikali  kuweka sera madhubuti pamoja na kutekeleza mikataba mbalimbali ya kimataifa ya  za huduma ya uzazi wa mpango na vijana hali itakayochangia kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia na nyanyasaji.
Mshauri wa shirika la Gender Link lenye Makao Makuu yake nchini Afrika ya Kusini Bi. Kubi Rama akitoa ufafanuzi wa jambo mapema jana katika ufunguzi wa Semina inayohusu maswala ya Afya ya Uzazi.

Afisa Programu ya Harakati na Ujenzi wa Nguvu za Pamoja wa TGNP Mtandao Bi. Anna Sangai akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mbele ya waandishi wa habari mapema jana jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taatisi ya Center Against Gender Violence  (CAGBV) Bi. Sophia Komba akichangia mada katika semina hiyo.


Washiriki wakifuatilia semina kwa umakini.

No comments