Ads

MANYANYA ,AWATAKA WANANCHI KUTEMBELEA MAONYESHO YA BIASHARA YA BIDHAA ZA NDANI





Naibu Waziri wa wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Eng. Stellah Manyanya. Akitazamabidhaa za kahawa katika bandari la kiwanda cha kukoboa kahawa cha mabinga, katika Maonyesho ya tatu ya biashara za bidhaa za ndani yanoyofanyika  viwanja vya Maonyesho vya Mwalimu Julius Nyerere Kulwa Road aliyekatikati ni Meneja Masoko wa kiwanda hicho David Amon Hauled.  (Picha na John Luhende)

Na.John Luhende 
Mwamba wa habari
Naibu wazir wa Viwanda na Biashara na Uwekezaji  Eng. Stellah Manyanya  , leo amefungua Maonyesho ya tatu ya biashara ya bidhaa za  Tanzania  yanayofanyika   katika viwanja vya Mwalimu Julius Kambabarage Nyerere na kusema kuwa     Wizara itaendelea kutafuta masoko ya bidahaa za Tanzania  katika masoko ya nje na kwamba kwasasa uagizaji wa bidhaa kutoka nje umepungua kwa kiasi  kikubwa hii nikutokana  na  kuongezeka kwa uazalishaji wa bidhaa kutoka viwanda vya  ndani na yanchi.


Akizungumza katika haflahiyo Manyanya  amesema , Wizara hiyo itaendelea kuratibu sekta ya viwanda na kilimo  na kuhakikisha kunakuwa na tija  kwa wakulima napia amesema wataendelea kuweka mazingira wezeshi na kuondoa vikwazo kwa wawekezaji  na mkakati kabambe umewekwa.

Amewataka washiriki wa maonesho hayo kutumia vizuri fursa ya soko huru na kuaacha tabia ya kuingiza biadhaa za magendo kwani inaathri biashara ya bidhaa za ndani  jambo ambalo likiachwa liatadumaza biashara , amesema Serikali imeendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kudhibiti wafanya biashara wasio waamifu ambao hulea bidhaa za magendo kutoka nje yanchi na kushusha bei ya bidhaa na kuathiri biagha ya ndani.

Katika Maonyesho ya tatu ya biashaya biadhaa za Tanzania na maadhimisho ya  siku ya viwanda Afrika, kumekuwa na ongezeko lawashiriki mwakahuu  ambapo viwanda  na Tasisi vimemefikia  513,mwaka huu kutoka wafanyabiashara 506, mwaka jana 2017.

Serikali ya awamu ya tano  chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli imeweka nguvu kubwa  katika ktekeleza sera ya  ya Maendeleo endelevu  ya Viwanda  (1996 -2020) awamu ya tatu  inayo tekelezwa kwa kipindi cha  2010 -2020 ambayo inatekelezwa kwa mkakati  unganishi wa maendeleo ya Viwanda na mpango wa  pili wa maendeleo ya miaka mitano 2016/17 -2020/21 moja ya malengo ya awamu hiyo  ambapo ni kuiwezesha sekta ya Viwanda  kuleta mabadiliko ya uchumi ili  kuiwezesha nchi  kufikia uchumi wa kati.

Pamoja na hayo amesema serikali imechukua jukumu la kununua korosho  ili kumlinda mkulima , na kuwaomba wafanyabiashara  wenye uwezo kusaidia kuagiza mashine za kubangua korosho  wafaye hiyo ili kuunga mkono  juhudi za serikali kumkomboa mkulima  .

“ Tunawahitaji wadau wa maendeleo kujitokeza kuwekeza katika korosho na si kuwalangua wakulima kwa beindogo napia nasisitiza watanzania tupende bidhaa zetu za ndani”alisema

Kwa upande wake  mwenyekiti wa Body ya TANRADE   Dkt Ngw’anza Kamata ,amesema  Tantrade kazi yake ni kuwatafutia masoko wafanya biashara  ndani nanje ya nchi  na kwamba yeye atasimamia maelekezo yote yanayo kuhusu biashara ili wafanya biashara waweze kunufaika  na pia Mamlaka hiyo itaendelea kuyatambua na kuyaainisha masoko ndani nan je kwaajili ya wafanyabiashara.

Amesema maonyesho ya biashara yanayofanywa na TANTRADE  yanalengo ya kuwakutanisha wafanyabiasha , wenyeviwanda na watumiaji wabidhaa ilikuona namna wanvyo weza kubadilishana mawazo na itasaidia kukuza biashara.


No comments