UWT KINONDONI USHINDI BILA RUSHWA KINONDONI INAPENDEZA
Na Heri Shaaban
Mwambawahabari
WANACHAMA wa Umoja wa Wanawake UWT wametakiwa kujiami na kupita kuomba kura kwa mgombea wao wa ccm jimbo la KINONDONI Maulidi Mtulia bila kutoa rushwa.
Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam Jana na Katibu Mkuu wa UWT Taifa Amina Makilagi wakati wa mkutano wa tathimini ulioandaliwa na UWT jimbo la Kinondoni .
" Wanawake wenzangu uchaguzi huu ccm tunashinda kwa kishindo kwa mgombea wetu Mauld Mtulia msitumie rushwa naomba UWT muwe Kifua Mbele tusubiri siku ifike apishwe aweze kusaidia wana Kinondoni na wanawake kwa ujumla" alisema
Makilagi aliwataka wanawake wa UWT kulinda shahada zao za kupiga kura siku ifike ya February 17 wajitokeze kwa wingi katika vituo kupiga kura.
.
Alisema jimbo hilo la ccm na litabaki kuendelea kuwa mikononi mwa ccm.
Aidha alisema MAENDELEO yanaletwa na ccm kwa kutekeleza ilani hivyo wasirubuniwe kupigia upinzani .
" Wanawake wenzangu wa jimbo hili wengi wajasiriamali hivyo Mara baada kuapishwa wasimamie waweze kupata mikopo ya wanawake na vijana" alisema
Aliwataka wana Kinondoni wamchague Mtulia kwani ni mnyenyekevu pia mwadilifu MTU mwenye maadili mazuri mwana zuoni .
Kwa upande wake Mgombea ubunge huyo Maulid Mtulia aliwapongeza wanawake wote wanaomuunga mkono pamoja na wana Kinondoni.
Mtulia aliwakikishia wananchi wa jimbo hilo kuwa yeye ni mchapa kazi sio mbabaishaji .
" Nichagueni changamoto zote nitasimamia ndani ya jimbo langu
Wanawake na wana Kinondoni tutashirikiana kukuza MAENDELEO."alisema Mtulia.
Post a Comment