Ads

RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA OFISI ZA BAKWATA, MUFTI ATOA NENO ZITO KWA WAISLAMU WATAKAO KWENDA KINYUME.

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akipeana mkono na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhaji Mussa Salum leo wakati alipokuwa akikagua ujenzi wa ofisi za BAKWATA.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akizungumza wakati wa ukaguzi wa ofisi za BAKWATA leo jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislamu pamoja na waandishi wa habari wakifatilia mazungumzo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry.
 Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry akizungumza na waandishi wa habari.
 Ujenzi wa Msikti mkubwa ukiwa unaendelea kujegwa katika Wilaya ya Kinondoni karibu na ofisi za BAKWATA. 
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akikagua ujenzi wa Ofisi za BAKWATA
Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry akiomba dua baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kumaliza ukaguzi wa ujenzi wa ofisi na msikti. (Picha zote na Noel Rukanuga)

.....

MWAMBA WA HABARI
NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM.
Viongozi wa dini nchini wametakiwa kuwa mstali wa mbele katika kufanikisha masula ya kimaendeleo ikiwemo ulipaji wa kodi pamoja na  kuliombea taifa ili liendelee kuwa na amani na uwajibikaji kwa watanzania wote.

Akizungumza leo wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa Ofisi za Baraza Kuu la Waislamu (BAKWATA) Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, amesema kuwa viongozi wa dini bado wana kazi kubwa ya kuhakikisha watanzania wanakuwa na amani na kuchangia katika ujenzi wa taifa.

Amesema kutokana umuhimu wa viongozi wa dini, serikali itaendeleo kuwapa ushirikiano ili kuhakikisha wanafanya kazi ya mungu katika mazingira rafiki.

“Nafasi ya Mufti ni kubwa sana hivyo tumeona ni vema kupatikana kwa ofisi kubwa ambayo itampa fursa ya kukaa faragha na mungu jambo ambalo ni jema katika kuhakikisha anatoa huduma kwa waumini ya dini ya kislamu katika mazingira bora” amesema Mhe Makonda.

Amesema kuwa mazingira ya ofisi ya awali yalikuwa sio rafiki kutokokana na kelele zilizokuwepo eneo hilo ambazo zilikuwa ni changamoto wakati Mufti Mkuu wa Tanzania akifanya kazi yake.

Makonda ameeleza kuwa makoa makuu ya BAKWATA yanapaswa kuwa na mazingira bora ili viongozi wa dini wanapokuja kutoka nchini mbalimbali waweze kufika sehemu mzuri.

“Pia kuna msikiti mkubwa unajengwa hapa nchini ambao unauwezo wa kuchukua waumni zaidi ya 6,000 ambapo utakuwa mkubwa kuliko yote afrika mashariki ”amesema Makonda.

Hata hivyo amefafanua kuwa baada ya kukamilika kwa ofisi hizo wataangalia namna ya kupiga hatua zaidi katika kuahakikisha BAKWATA inakuwa na maendeleo.

“Naomba BAKWATA mnipe orodha yote ya viwanja ambavyo umedhulumiwa ili muweze kuvipata na kufanya maendeleo” amesema Makonda.

Kwa upande wake Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubeiry bin Ally amemshuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha ujenzi wa ofisi za BAKWATA.

Amesema kwa muda wa miaka 50 mpaka sasa BAKWATA haijawai kuwa na ofisi kubwa ambayo ni rafiki katika kuhakikisha wanafanya kazi zao.

“Tulikuwa tanapata changamoto kubwa pale tunapoona viongozi wa dini kutoka nje ya nchi kuja kututembelaea kutokana na ofisi zetu kuwa na mazingira sio rafiki kwani kuna kelele zinazotokana na sauti za watu wanaoishi na kufanya biashara karibu na ofisi zetu " amsema Mufti Zubeiry.

Amesema kutokana hali ujenzi huo ambao unaendelea vizuri ni jambo jema kwa BAKWATA, huku akiwataka waumini wa dini ya kislamu waendelee kufanya kazi ya mungu kwa umakini na kujiepusha na mambo ambayo sio rafiki.

“Kiongozi wa dini ya ambaye atakwenda kinyume na BAKWATA tutamtumbua ili sisi tuendelee mbele na sio kuturudisha nyuma” amesema Mufti Zubeiry.

Hat hivyo Mufti Zubeiry ameeleza kuwa wanaendelea kumuomba mungu ili mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na serikali kwa ujumla waendelee na mpango wa kufanikisha maendeleo ya nchi.

“Waislamu tutaendelea kuliombea taifa na kukumbushana uwajibikaji kwa waumini wetu ili tuzidi kusonga mbele na kufanikisha maendeleo ya taifa kwa ujumla” amesema Mufti Zubeiry.

No comments