Ads

CCM ILALA YAAZIMISHA MIAKA 41 YA CCM, KWA KUTOA MSAADA, WAKUBALI KAZI ZA MAKONDA


Mwambawahabari
MWENYEKITI wa Wilaya ya Ilala kupitia chama Cha Mapinduzi (CCM) Abulaziz Juma amewataka wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka ya kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) ili kuweza kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais John Magufuli.

 Agizo hilo amelitoa Jijini Dar es Salaam  wakati alipokua katika sherehe za kutimiza miaka 41 kwa chama hicho ambapo amesema Serikali imekua ikifanya jihudi mbali mbali katika kuzuia na kupambana na Rushwa ili kuweza kuleta maendeleo.

Aidha amewataka wananchi waendelee kumuombea Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ,Poul Makonda amekuwa akifanya juhudi mbalimbali kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo ya haraka hivyo ni vyema Rais akaendelea kumueka katika mkoa huo ili kuweza kuitangaza vyema ilani ya chama.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Buguruni Mivinjeni Barua Mwakilanga kwa kushirikiana na Mjumbe wa Mkutano mkuu wa Jumuiya ya Wazazi. Dkt Mohammed Honelo wamesema , wameamua kutoa msaada huo kutokana na kuunga jitihada za Serikali ikiwa ni pamoja kutekeleza ilani ya chama.

Ameongeza kuwa, ilani ya chama hicho hakikatazi mtu kutoa msaada sehem yoyote, hivyo walipokea maombi kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa Nyeburu  hivyo akaamua kutoa msaada wa bati 60 ambapo 40 ni kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya chama kwa mtaa wa Nyeburu A na B na bati 20 kwa ajili ya Msikiti.

No comments