Ads

MAKONDA ALIVALIANJUGA TATIZO LA UTAPELI WA ARDHI NA MAJUMBA DAR,ATOA AGIZO ZITO KWA MATAPELI NA WALIOTAPELIWA

Image result for picha za makonda

Mwambawahabari
Mkuu wa Mkuu wa Dar es salaam Paul Makonda amewatangazia wananchi wote wa Mkoa wa Dar es salaam waliodhulumiwa mali zao ikiwemo viwanja, nyumba, mashamba, magari na vifaa vingine kufika ofisini kwake.

Makonda amewataka watu hao kufika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ilala Boma kuanzia January 29 hadi February 02 kwaajili ya kupatiwa msada wa kisheria.

Mkuu wa mkoa huyo amefunguka hayo leo na kusema kuwa amewaanda wanasheria magwiji wa kutosha kwaajili ya kusikiliza matatizo na changamoto za wananchi na kudai wananchi wanapaswa kufika na nyaraka na vielelezo halali ili wapatiwe haki zao.

Makonda ameamua kufanya hili baada ya kubaini uwepo wa baadhi ya wananchi wanyonge wanaodhulumiwa mashamba, mali zao na kunyanyasika kwa kuporwa haki zao na watu wenye uwezo kifedha au wanasheria wenye utaalam wanaokandamiza wanyonge.

No comments