Ads

MBUNIFU WA JIKO LA GES LA GHARAMA NAFUU ALIYE PANIA KUNUSURU MISITU NA MAZINGIRA AWATAKA WATANZANIA KUACHANA NA KUNI NA MKAA.


Na John Luhende 
mwambawahabari
Dunia sasa inapita katika mabadiliko ya hali ya tabia ya nchi ambapo hali hiyo kwa mujibu wa wataalaamu wa mazingira wanasema hali hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za kibinadamu.

Shughuli hizo ni pamoja ukataji miti holela kwaajili ya mbao , kuni ,mkaa na shughuli za kilimo ambazo hufanywa katika vyanzo vya maji, ukiacha uchafuzi mwingine ambao hufanywa na viwanda vikubwa ambavyo navyo huzalisha hewa ya ukaa na kemikali ambazo huchafua hewa na vyanzo vya maji na kuathili viumbe hai na mimea.


Inocent Kazungu ni  mwanamazingira na mbunifu wa jiko sanifuni ambalo hutumia ges, anasema suala la kutunza mazigira ni muhimu sana

“Nimebuni jiko jiko hili nimelipa jina la Cooker take away na jiko lapilli nimelipa jinala Kazungu ges (mwendo kasi) majiko hayo yana rahisisha sana kazi za kupika na nigharama nafuu sana mtungi wake mgogo ni kuanzia shilingi 2000tu. naomba watanzania tuachane na kuni na mkaa tutunze mazingira yetu” Alisema mbunifu huyo.

Amesema lengo la kubuni hili jiko ni kuokoa misitu ambayo kila siku ime endelea kuteketea kwaajili ya kuni na mkaa wa kupikia  na sasa jiko hili lita kuwa mbadala  wa nishati nhiyo na lina tumia gesi asili ya hapahapa nchi na anashukuru serikali kwa kutambua  mchango wa wabuni wa majiko na wanachi wameelewa kuwa nia yetu ni njema kuokoa misitu yetu .

“Naishukuru serikalikupitia NEMC  imenipeleka sehemu nyingi sana ikiwemo katika maonyesho ya sabaaba Dar es salaam , Nanenane Lindi na katika siku ya mazingira Dunian ambayo yalifanyika   Butiama katika mkoani Mara na kote huko nimetoa elimu ya kutunza mazingira na matumizi ya jiko langu na nina shukuru sana watanzania wamelipokea kwa vizuri na mahitaji yamekuwa makubwa” alisema Kazungu

Pamoja na hayo anasema changamoto kubwa kwa wabunifu wa kitanzania imekuwa ni mtaji wa kuendeleza ubunifu wao  anasema anapata wateja wa majiko kutoka mikoa mbali mbali laiki anashindwa kukidhi mahitaji ya soko kwa kuwa hana mtaji wa kutosha lakini anaimani kuwa kwa kipindi hiki ambapo serikali inahimiza kuanzisha kwa viwanda watapata uungwaji mkono kutoka serikalini ili kuwaeza kuwa na viwanda vidovidogo.


Kwa mahitaji yako ya jikobora  la ges   lenye gharama nafuu Kazungu anapatikana  Vingunguti sido au wasiliana naye kwa companykazungu@gmail.com na 0673899222.


No comments