WAZIRI SIMBACHAWENE KUOMBA JIJI LA DODOMA KWA RAIS JOHN MAGUFULI
Mwambawahabari
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais 
TAMISEMI George Simbachawene (wa pili kushoto) akiingia katika Ofisi za 
Mhandisi wa Halmashauri ya  Manispaa ya Dodoma kukagua magari na mitambo
 iliyorithiwa na Manispaa hiyo kutoka kwa iliyokuwa Mamlaka ya 
Ustawishaji Makao Makuu (CDA) wakati wa ziara ya siku moja ya  Waziri 
huyo katika Manispaa hiyo jana. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma 
Christine Mndeme na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma 
Mhandisi Lusako Kilembe. 
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya 
Dodoma Mhandisi Lusako Kilembe (kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi
 Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene wakati wa ziara ya siku moja
 ya  Waziri huyo katika Manispaa hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya 
Dodoma Christine Mndeme
………………………………………………………………………….
Na Ramadhani Juma
Ofisi ya Mkuruygenzi wa Manispaa
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais 
TAMISEMI George Simbachawene ameahidi kumfikishia Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli ombi la kuitangaza Manispaa ya 
Dodoma kuwa Jiji kwani inakidhi vigizo na kwamba sasa ni wakati muafaka 
wa kupewa hadhi hiyo.
Alitoa ahadi hiyo jana wakati 
akizungumza na watumishi wa Manispaa ya Dodoma katika Ukumbi wa Shule ya
 Sekondari ya Dodoma ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku moja katika 
Manispaa hiyo, iliyojumuisha pia ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo.
Aidha, amewataka watumishi wa 
iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao (CDA) kumshukuru Rais kwa uamuzi 
wa kuivunja Mamlaka hiyo kwa sababu hatua hiyo imeondoa mkanganyiko 
uliokuwepo katika kuhudumia wananchi hususani katika sekta ya ardhi na 
mipango miji ambako Manispaa ya Dodoma pia ilikuwa na jukumu hilo.
Pia aliwaeleza watumishi hao 
wapatao 260 kuwa, sasa watapata fursa pana zaidi ya kuitumikia nchi yao 
katika mikoa mbalimbali watakayopangiwa kuendelea kutumikia wananchi 
kwani wao ni watumishi wa umma na wana haki na wajibu wa kufanya kazi 
sehemu yeyote nchini.
 
 
 
 
 
Post a Comment