Ads

Vijana nchini washauriwa kujiajiri kupitia Sanaa.



Na Shamimu Nyaki- WHUSM.
mwambawahabari
Katika kukabiliana na upungufu wa ajira hapa nchini Vijana wameshauriwa  kujiajiri  kupitia Sanaa na vipaji walivonavyo katika kupata kipato.
Ushauri huo umetolewa jana Wilayani  Bagamoyo na Kaimu Mkurugenzi  Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi alipokuwa anawahutubia wahitimu wa Astashahada na Stashahada  ya Sanaa na Ufundi katika Chuo cha Sanaa na Ufundi  Bagamoyo  kilichopo  chini ya Taasisi ya Sanaa  na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).
“Tumieni elimu mliyopata   kujiajiri wenyewe ili kuepuka changamoto ya ajira iliyopo hapa  nchini, ujuzi mliopata  ni njia pekee ya kujiletea kipato na Taifa kwa ujumla”.Alisema  Bibi Leah.
Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa  wasanii wote wanaofanya kazi za Sanaa ni vyema wakasajili  kazi zao katika Mamlaka husika  ili iwe rahisi kwa Serikali  kutoa msaada kwa urahisi kwaWasanii hao.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu waTaasisi ya Sanaa na Utmaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt.Herbet Makoye aliwasihi  wahitimu hao kuwa mabalozi  wazuri wa sanaa  watakapokuwa wanafanya shughuli zao za Sanaa.
“Nendeni mkawe mabalozi  wazuri wa Chuo  chetu kwa kuwa Wasanii  bora na kutengeneza  kazi nzuri ili muweze kushindana  na soko la ajira”. Alisisitiza Dkt.Makoye.
Naye mhitimu wa ngazi ya  Stashahada ya Sanaa na  Ufundi  Bi Imelda John amesema  kuwa elimu aliyoipata itamsaidia  kufanya kazi ya Sanaa kwa weledi zaidi hasa katika  fani ya kutengeneza Filamu na Picha Jongefu.
Mahafali hayo ni ya 27 katika chuo hicho ambapo kwa mwaka huu jumla ya wanafunzi 85 wametimu Astashahada na Stashahada ya Sanaa na Ufundi.

No comments