Ads

UCHAGUZI WA MEYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM FIGISUFIGISU,WAVUNJIKA TENA ,POLISI WATANDA KILA KONA UKUMBI WA KARIMJEE,UKAWA WAHAHA.

mwambawahabari blog

VURUGU kubwa zimetokea wakati wa Uchaguzi wa meya wa Jiji la Dar es Salaam,mara baada ya uchaguzi huo kuhairishwa  tena k wa mara ya nne leo,huku Jeshi la Polisi likivamia ukumbi wa Karimjee na kuanza kupambana na Madiwani na wabunge wa Muunganiko wa umoja wa Vyama vinavyounda  UKAWA.

Tukio hilo la aina yake limetokea leo  Jijini  mara baada ya mkurugenzi wa Jiji kutaka  kuaharisha  uchaguzi huo kwa madai kuwa  uchaguzi huo ume wekewa  pingamizi mahakamani , jambo hilo likawachukiza  madiwani wa UKAWA wakidai kuwa hawajapata barua  kuhusu  kesi hiyo.

Mara baada ya UKAWA kugomea hoja hiyo ndipo wakafikia hatua ya   kutaka kufanya uchaguzi wenyewe huku wakisema   ahadi ya madiwani kufanya uchaguzi imetimia na wakaomba waendelee kufanya uchaguzi huo.

Wakati wakijiiandaa kufanya uchaguzi huo ukawa wenyewe ,ndipo Polisi zaidi ya 15 wakavamiaka ukumbi huo na kuwataka kuwakamata madaiwani wa ukawa ili waondoke ukumbini kuzuia uchaguzi usifanyike,jambo lilowachukiza tena ndipo Polisi wakaanza kuwatuliza   madiwani wa Ukawa .


credit fulhabari

No comments