SIMBA NA YANGA ZATOSHANA NGUVU, SIMBA WASHANGILIA
MECHI ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara baina ya watani wa jadi, Simba na Yanga imemalizika kwa kutosha nguvu ya bila kufungana mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Timu zote zimecheza mchezo mzuri dakika zote mbili hadi mwamuzi anapuliza kipyenga cha mwisho watani hao wamegawana alama moja moja.
Kwa Matokeo hayo Yanga wameendelea kuongoza Ligi hiyo kwa kufikisha Pointi 20 huku Simba wakibaki nafasi ya pili kwa pointi 18 baada ya timu zote kucheza mechi nane.
Pamoja na hayo itakumbukwa kuwa Watani hao mwaka huu wamekutana mara Tano Yanga Ikishinda mara Tatu Simba mara moja na Leo Timu zimetoshana nguvu, huku mashabikibwa Simba Katika uwanja wa Mkapa wakionekana kushangia Zaidi matokeo ya Leo .
"Naitwa Ally Musa nishabiki wa Simba kindaki ndaki , nashangila matokeo ya Leo kwakuwa mwanzo wa mchezo Yanga walikuwa wanapewa nafasi kubwa ya kushinda , nakweli ukiangalia sisi Simba hatunatimu nzuri msimu huu ukilinganisha na wenzetu " Alisema shaki huyo
Post a Comment