Ads

TPB YATOA MSAADA WA FIMBO NYEUPE KWA CHAMA CHA WASIOONA DSM

Mwambawahabari

Benki ya TPB, imetoa msaada wa fimbo nyeupe 20 kwa chama cha wasioona tawi la Dar es Salaam, zenye thamani ya sh milioni 1. Msaada huo ulitolewa jana na Meneja wa Mawasiano wa Benki ya TPB, Bi. Chichi Banda na kukabidhiwa Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Seif Jega. 

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Bi Chichi Banda alisema benki hiyo ilitoa msaada huo kama sehemu ya utekelezaji wa majukumu yake katika jamii. 

‘’Katika uendeshaji wa benki yetu, huwa tuna utaratibu wa kutenga kiasi cha faida kila mwaka kwa ajili ya kusaidia jamii katika maeneo makuu matatu ambayo ni afya, elimu na ustawi wa jamii’’. 

Hivyo basi tunawaomba wananchi muendelee kutuunga mkono kwa kutumia huduma zetu za kibenki kwani tunachokipata kama faida, mara zote tumekuwa tukirudisha kwenu kupitia misaada tunayotoa’’, alisema Chichi.

 ‘’Tunaamini msaada huu, utaenda kupunguza changamoto kwa wale wasioona ambao walikosa kifaa hiki muhimu katika maisha yao’’, aliongeza Chichi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Seif Jega, aliushukuru uongozi wa benki ya TPB kwa msaada huo ambao utawasaidia katika maadhimisho ya Siku ya fimbo cheupe dunia utakaofanyika kitaifa mkoani Mwanza siku ya tarehe 25 Oktoba 2018.

Katika maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajia kuwa Makamu wa Raisi, Mhe. Mama Samia Suluhu. ‘’Kwa kweli tumefarijika sana, kupokea huu msaada kutoka benki ya TPB, na tunaahidi tutaufikisha kwa wanachama wale ambao walikuwa hawajapata bado fimbo hizi’’, alisema Jega. 


No comments