Ads

MEYA KUYEKO, AFURAHISHWA NA KAZI YA MASHAMBA DARASA YA ILALA NANENANE MOROGORO.


 Na. John Luhende
 Mwambawahabari 
Mstahiki Meya  wa Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko amewapongeza Wakulima na wadau wa Kilimo wa Manispaa ya Ilala kwa kazinzuri waliyoifanya katika shamba darasa la Manispaa hiyo lililopo hapa mjini Morogoro katika viwanja vya nanenane.
 Kuyeko ameyasema hayo baada ya kutembelea shamba darasa la Manispaa hiyo ambapo amejiionea shughuli za Wakulima , wafugaji na Wajasiliamali wa mazao ya kilimo na Mifugo  wanaoshiriki maonesho wa Wakulima katika viwanja vya nanenane mjini hapa.
 "Wamefanya kazi nzuri napenda niwashukuru wadau wetu  nimeona mlivyo jipanga naona hapa  na kaulimbiu ya mwakahuu inayosema, Wekeza katika kilimo, katika Viwanda na katika uvuvi kwa maendeleo ya viwanda  wametekeleza ipasavyo" alisema.

 Amesema, Nanenane ya mwakahuu imekuwa bora na kueleza kufurahishwa  kwake na kilimo cha Uwiano kinatumia mazingira, na kilimo cha mbogamboga na mazao mengine na kusema kuwa kunatija katiki kushiriki  maonyesho hayo ukilinganisha na miaka iliyopita.
 Naye Afisa kilimo wa Manispaa ya Ilala sija Hadson Sije, amewakaribisha wananchi wote kutembelea shamba Darasa la Ilala ili we wezesha kujifunza mbinu mbalimbali za kilimo hasa kilimo cha mjini.

 "Ilala iko mjini tumekuja kuonyesha namna pia ambavyo wananchi wanaoishi mjini wanaweza kutumia eneo dogo kwa kulima na kuotesha michezo ya mbogamboga na wakipata mbogamboga bora zisizo na kemikali kwa kutumia mbolea ya asili" alisema


Kwa upande wa ufugaji wanaonea namna ya kufunga samaki, kuku, bata, Sungura ng'ombe na mbuzi.











No comments