Ads

"WANA WAKE WAWEZESHWE KUFANYA BIASHARA NA MIRADI MIKUBWA SIYO BATIKI NA UREMBO PEKEE" DC MJEMA.





Na John Luhende
Mwambawahabari
Mlezi wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala mhe. Sophia Mjema amelitaka Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi  JUWADA kuwa fundisha wanawake kuwa serikali inayo mifuko 19   ya kuwa wezesha kiuchumi ambayo wanaweza kuitumia ili kujiendeleza kibiashara.


Mjema Ameyasema sema hayo  katika  mkutano wa semina ya Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam iyofanyika Mlimani City, na kuongeza kuwa wanawake wanao uwezo mkubwa wa kuendesha biashara  kubwa na uwekezaji katika  Kilimo, Madini  na Uvuvi  ikiwa watawezeshwa kupata mitaji.

"Wanawake hawa wanataka kuwezeshwa  ndiyo maana wako hapa  Katibu wangu naomba muwafundishe kuwa serikali ya awamu ya tano inayo mifuko 19,wawezesheni kwenye mifuko ya kilimo, Bara Bara, hata uvuvi mwanamke anwezakumwajiri mtu na aka fanya shughuli za uvuvi, tusiwaachie wanaume tuhizi kazi hizi  wanawake tuna weza"Amesema

Aidha  amesema imefika wakati wanawake kufanya biashara na miradi mikubwa na sikila wakati Wana an zishatengwa biashara la batiki, na Sabuni tu.

"Tunataka  wanawake watakao kuwa kama Maida, wajenzi  wa mabarabara na taifa hili  lita piga  hatua kubwa ikiwa wanawake tutawawezesha  na wasiwe tegemezi kwa Wanaume tu hii ndiyo dhamana ya Kiongozi wetu aliye anzisha majukwaa haya Mama Samia Suluhu" Amesema.


Kwa upande wake Mgeni rasmi katika Mkutano huo ambaye ni Naibu Waziri wa Viwanda biashara, na uwekezaji Mhe. Stella Manyanya  amewataka wanawake kutumia fursa zilizotolewa na serikali, mikopo na Elimu ya ujasiriamali mali inayo tolewa ilikujiendeza kiuchumi.

Hata hivyo ametoa wito kwa Wanawake hao wajasiriamali  kupata elimu ya kutosha na kuona umuhimu na kujiunga kupata nembo  za Simbo  milia ambazo zita wa tambulisha katika biashara  kitaifa na kimataifa.

"Natoa agizo  tunakaribia kuanza maonesho ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya saba saba Mkurugenzi ahakikishe anaendeakutenga nafasi za kutosha kwa wajasiriamali wa ndani. Amesema.

No comments