Ads

SERIKALI YATANGAZA NEEMA KWA WAKULIMA WA PAMBA YAFUTA DENI LA VIUADUDU.

Image result for picha ya Dkt Charles Tizeba
NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA

SERIKALI imefuta mikopo ya wakulima ya viuadudu vyote vilivyotumika msimu huu katika zao la pamba nchini na badala yake Mfuko wa Wakfu wa Kuendeleza zao la Pamba utalipa madeni hayo.
Kauli hiyo imetolewa leo(jana)wilayani  Igunga na Waziri wa Kilimo Dkt . Charles Tizeba wakati wa sherehe za uzinduzi wa msimu wa ununuzi wa pamba kwa mwaka 2018/19 ambapo kilo moja itanunuliwa kwa shilingi 1,100/-.
Alisema wakulima wa pamba ambao wameshiriki katika kilimo cha mkataba watalipa mbegu na sio viuadudu ambazo alikopeshwa na Kampuni mbalimbali.
Dkt. Tizeba aliongeza kuwa wakulima ambao walinunua kwa kutumia fedha zao hatalipa chochote.
Aidha Waziri huyo aliongeza kuwa katika msimu ujao wa kilimo wa 2019/20 hakutakuwepo na kilimo cha mkataba bali Mfuko wa Wakfu wa Kuendeleza zao la Pamba utaviwezesha vyama vya Ushirika vya Msingi kupata pembejeo kwa ajili ya wakulima wote nchini.
Alisema wakulima watapatiwa mbegu na viuadudu bure kulingana na uwezo wa mkulima kulima ili waweze kuongeza uzalishaji wa zao hilo.
Aidha Dkt.Tizeba aliiagiza Bodi ya Pamba nchini kushirikiana na Mahakama ili waweze kuwa na Mahakama inayotembea(Mobile Court ) ili kudhibiti ubora na wizi kwa kutumia mizani.
Alisema AMCOS yoyote iytakayobainika kuchezea mizani au kununua pamba chafu ichukuliwe hatua.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri aliwaonya viongozi wote wa Vyama vya Ushirika vya Msingi ambao wamejiingiza katika uongozi kwa nia ya kuwaibia wakulima waondoke mara moja la sivyo watakumbana na mkono wa Sheria.
Alisema hatakubali kuona mkulima anaibiwa kwa kutumia mizani ya rula au kukata kilo na kuongeza kuwa ushirika wa hivi sasa ni mahali patakatifu.
Mwanri aliongeza kuwa kiongoza aliyepo madarakani ni lazima ajihakikishie kuwa yeye ni msafi na kama ana rekodi ya wizi ni vema akaondoka mwenyewe kabla hayamkamata na kumweka ndani.
Alisisitiza kuwa hawezi kusubiri wakulima waibiwe ndio hawakamate viongozi hata akisikia fununu za wizi atalazima kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sharia.





No comments