Ads

WAZIRI UMMY MWALIMU KUWA MGENI RASMI HEALTH SUMMIT


Na Rayusa Yasini. 
Mwambawahabari
WAZIRI wa Afya  jamii ,jinsia, wazee na watoto  anatarajiwa kufungua kongamano la Tatu la Kitaifa la afya lijulikanalo kwa jina la  Tanzania Hearth Summit.

Akizungumza Leo jijini Dar es Salaam Rais wa kongamano hilo Dr Omar Chino amesema mada mbalimbali zitazungumzwa kutoka kwa washiriki 142 ambao mpaka sasa wamethibitisha ushiriki wao.

Chino amesema sheria za usalama na afya makazini, kanuni na ufanyaji kazi katika Tanzania na hali ilivyo kwa sasa pamoja na nini kifanyike ili kuboresha hali ya afya.

Kuelekea kwenye huduma ya afya kwa wote, mchango wa taasisi za uma na binafsi zitaongelewa ili kuona jinsi tutakavoendelea.
"Mpango wa kuelekea kuwa kituo cha ubora katika magonjwa ya moyo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ".

Ameongeza kuwa jitihada za Tanzania za kufikisha malengo ya maendeleo ya kimkakati ya maisha yenye afya njema yatazungumzwa kwa pamoja na kupata muafaka.

Kongamano la afya litafanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere utakaozihusisha taasisi za MoH ,TMHS, na Baraza la kiislam Tanzania BAKWATA.huku wadau wa afya wakiombwa kuendelea na usajili kupitia WWW.ths.or.tz.

Mkutano  huo ambao utakutanisha taasisi 53 za afya, zinatarajia pia  kushiriki katika maonesho  ya bidhaa zinafanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia , Wazee na Watoto pamoja na TAMISEMI tangu kuanza kwake 2014.

No comments