Ads

KURASINI SDA KWAYA WAPATA VYOMBO VIPYA VYA MUZIKI

mwambawahabariblog

Na John   Luhende
mwambawahabariblog
Katika kuhakikisha  Injili ya Yesu kristo ina hubiriwa kwa  mataifa yote watu  watatu ambao majina yao tumeya hifadhi  wameonekana kuwa ni wenye mapenzi mema na kazi ya Mungu    wamejitolea kununua vyombo vya  muziki PA SYSTEM katika kanisa la Waadventista Wasabato  kurasini  ambapo vyombo hivyo  vina thamani ya shilingi milion  saba na laki tatu ,vitatumika na  kwaya ya kanisa hilo ambayo ina julikana kama  Kurasini SDA Kwaya , au kwajina la utani  (Fuso).

Akiendesha huduma ya kuweka waqifu vyombo hivyo mzee wa kanisahilo   Joseph Nganga ,  amewaomba wasamaria wengine kuguswa na kazi ya Mungu na kuendelea kuchangia kwakuwa bado kuna upungufu wa vyombo   vya muziki nakuwataka kutambua uthamani wa kwaya hiiyo,akitoa mfano wa kujulikana kwa kwaya hiyo mzee Nganga alisema


“ majuma machache yaliyopita  mama mmoja kutoka mwanza alikuwa akitafuta  kanisa lakwaya hiyo  lilipo   iliaje kusikiliza nyimbo na kuchangia fedha kwaajili  ya huduma kwa kazi ya Mungu,  alipata taabu sana kuwakuwa alikuwa hapafahamu mahali lilipo kanisa , alipotea lakini mwishowe alifika ,   hii inaonyesha ni namna gani kazi hii ya waimbaji ilivyo wafikia watu wengi haijalishi wako umbali kiasi gani “ alisema mzee nganga.


Katika hatua nyingine kanisa hilo  kufuata utaratibu wa kanisa la  Wasabato ulimwenguni  washiriki wa kanisa la   Wasabato kurasini  wameingia katika mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es salaam kugawa vitabu 270 vikiwemo vya TUMAINI KUU  pamoja na vitabu vya SABATO YA KWELI  na badhi ya vipeperushi (vijizuu)  ilikupeleka injili kwa watu wote  wamfahamu Kristo  waache dhambi  wamchemungu waokolewe .

No comments