Ads

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani ajiuzulu




 BERLIN

Mwamba wa habari

Waziri wa Ulinzi nchini Ujerumani Christine Lambrecht amejiuzulu.

Lambrecht ametowa taarifa ya kujiuzulu leo Jumatatu akisema kwamba amewasilisha ombi lake hilo kwa Kansela Olaf Scholz na kuongeza kwamba miezi kadhaa ya kumulikwa kwake na vyombo vya habari kumeondowa mjadala wa kweli kuhusu jeshi na sera ya usalama ya Ujerumani. 

Waziri huyo wa ulinzi wa Ujerumani ambaye amekuwa akikosolewa kuhusu hatua zake kuelekea Ukraine,amesema kazi muhimu ya wanajeshi na watu wengi kwenye wizara yake inapaswa kupewa kipaumbele.

 Hatua ya kujiuzulu Lambrecht imekuja katika kipindi nyeti ambacho Kansela Scholz anakabiliwa na shinikizo kubwa la kumtaka achukue hatua nyingine kubwa ya kuipatia msaada wa kijeshi Ukraine.

Chanzo DW

No comments