Ads

RC SINYAMULE AWATAKA WANAFUNZI ,WAZAZI KUTAMBUA UMUHIMU WA MAZINGIRA

 



Mkuu wa mkoa wa dodoma Rosemary Sinyamule amewataka wazazi na walezi   kuhakikisha wanawapeleka watoto  wao shuleni   mara baada ya shule kufunguliwa.

Senya Mule ameyasema hayo    katika ziara ya Kampeni ya upandaji wa miti iliyofanyika katika hospital ya wilaya ya chemba jijini dodoma ambapo pia amewasihi wananchi  kupanda miti  Kurudisha uoto  wa asili Ili kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi.

Sinyamule amesema kuwa zipo Sheria ambazo inalazimika kufuatwa kuhakikisha kuwa mtoto anapata haki yake ya kwenda shule hivyo inapaswa wazazi na walezi watambua  lengo na makusudi ya serikali ya awamu ya sita kwa watoto wa kidato Cha kwanza.

Aidha amesema kuwa yapo maelekezo ambayo yametolewa na serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha  mazingira yanatunzwa ,hivyo ni jukumu la kila mwanafunzi kuwa na mti wake shuleni ambao atautuza kwa kipindi chote awapo shuleni na wazazi watambue kama elimu ya vitendo.


No comments