DC DKT MJEMA AHAMASISHA WANANCHI KUHUSU KUJIKINGA NA UGONJWA WA CORONA .
Na John Luhende
Mwamba wa habari
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Dkt Sophia Mjema leo amewataka wananchi wa Wilaya ya Ilala na wale wanaoingia wilayani humo kuzingatia kanununi za afya na maelekezo ya wataalam wa afya ili kuweza kujikinga na ugonjwa wa CORONA.
Dkt Mjema ameyasema hayo leo wakati wa ziara ya kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kujikinga na ugomjwa wa Colona unaoenezwa na Virurusi vya COVID 19 .
Aidha DC Dkt Mjema ametembelea maeneo ya Kariakoo sokoni,Bandari ya boti za kwenda Zanzibari,Soko la Ferry na maeneo mengine yenye mikusanyiko na kuhamasisha wananchi kunawa mikono kwa dawa maalumu ambapo pia aliwanawisha .
"Tunawaagiza wasimamizi wa vyombo vyote vya kubeba abiria kwamba zoezi hili niendelevu wahakikishe wanasafisha kwa dawa vyombo vyao"Alisema
Kwa upande wake Afisa afya wa Manispaa ya Ilala Reginald Mlai , amesema kunawa mikono pekee haitoshi ila wananchi pia wanatakiwa kufunika midomo wakati wa kukohoa.
Nao baadhi ya wananchi waliopewa elimu hiyo wamemshukuru Mjema kwa kwa kuwajali wananchi huku wakiomba Serikali kuongeza juhudi katika ktoa elimu kwani wananchi wengi hawanauelewa kuhusu ugonjwa huo.
"Sisi wafanya biashara ndogondogo tunaomba Rais atufanyie mpango wa kununua maski maaana zimekuwa beighali sana"alisema mmoja wa wafanyabiashara ndondogo Kariakoo.
Post a Comment