OLE NASHA ATAKA WADAU SEKTA YA UTALII KUSHIRIKIANA
Mwambawahabari
NA Maria Kaira,Mwambawahabari
NAIBU Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Ole Nasha, amezitaka Taasisi za mafunzo
na wadau wa sekta ya Utalii kufanya kazi
kwa weledi pamoja ili kutatua changamto zilizopo ili kufikia uchumi wa kati
ifikapo mwaka 2020.
Akizungumza
na wadau hao jijini Dar es Salaam wakati
wa kufunga Kongamano la Kimataifa la kuunganisha wanataaluma na wadau wa sekta
ya Utalii na Ukarimu ambapo amesema kama taifa ni lazima kuwekeza katika
utayarisha wa vijana wakitanzania ili
kupata nguvu kazi yenye weledi na umahili wa kutosha katika sekta ya utalii.
Ole Nasha amesema kumekuwepo na ushindani mkubwa katika
soko kutokana na kuongezeka kwa
wataalamu hao hivyo kunahitajika maandalizi mazuri ya rasilimali watu ili
kuweza kushindana katika soko la dunia.
“Sekta ya
Utalii ni moja ya Sekta inayoipatia Taifa fedha za kigeni kutokana na utalii
hivyo kukiwa na nguvu kazi yenye weledi
na ufanisi wa kutosha nchi itaneemeka kupitia utalii na taifa litakuwa la mfano”amesema.
Aidha
amesema Tanzania ni nchi ya pekee iliyojaliwa kuwa na rasilimali nyingi, nchi
jirani zimepiga hatua kwenye kuvutia watalii sio kwamba wana vivutio vingi
kuliko sisi ni kutokana na mambo mengine kuwa na nguvu kazi yenye weledi ndio
maana kama Taifa tunawekeza katika kutayarisha vijana ili kuwa na nguvu kazi
yenye weledi katika sekta ya utalii,” alisema na kuongeza.
.
Hata hivyo
amevipongeza chuo cha Taifa cha Utalii na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa
kuandaa mkutano wa kuwaunganisha wakufunzi na watoe huduma hiyo walio katika
biashara ya Utalii kwani kwa pamoja wanaweza kutatua changamoto zilizopo.
Naye Mkuu wa
Chuo cha Taifa cha Utalii, Dkt. Shogo Mlozi amesema kwa kushirikiana na vyuo
vingine vinavyotoa mafunzo ya utalii wataendelea kuimarisha mpango wa utoaji
mafunzo kwa kufanya kazi karibu na watoa huduma ili kupata nguvu kazi yenye
weledi na ujuzi.


Post a Comment