Ads

Meya Kumbilamoto ahimiza vijana kushiriki michezo.


Mwambawahabari

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akizungumza na vijana wa Timu ya Mpira Vingunguti leo asubuhi.

Kumbilamoto ametumia nafasi hiyo kuwashukuru Vijana hao na wananchi wa  Ilala kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha  katika Daftari la wapigakura kwaajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019.

"Michezo ni Afya,Udugu,na pia niajira  nahimiza Vijana tupende michezo  natuendelee kushirikiana nami nitakuwa nanyi bega kwa bega" Alisema Kumbilamoto.

Pia amewakabidhi  mpira na kuwataka vijana hao wazidi kumuombea dua Rais Magufuri kwa kazi kubwa anayoifanya yakujenga nchi.

 Akishukuru kwa niaba ya wachezaji kiongozi wa Timu hiyo amemshukuru Meya kwa kuwatembelea nakuwapa Mpira  na kusema kuwa kabla ya mpira huo walikuwa wakikodi kwa Mtu.

No comments