RC MAKONDA ATOA MWEZI MMOJA KWA MANISPAA YA KINONDONI KUANZA UJENZI WA FUKWE ZA COCO.
Mwamba wa habari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Mhe. Paul Makonda leo August 09 ametoa Mwezi Mmoja kwa Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Kinondoni na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kuhakikisha ujenzi
wa maboresho ya Fukwe za Coco unaanza mara moja na kama wakishindwa watanyang'anywa
fedha hizo na kutafutwa mzabuni.
Mapema leo RC Makonda
akiambatana na Katibu Tawala wa mkoa huo wamefika kwenye ufukwe huo kwaajili ya
kuangalia maendeleo ya mradi lakini wameshangazwa kuona hakuna chochote
kinachoendelea wakati tayari Rais Dkt.John Magufuli alishatoa kiasi cha
Shilingi Bilioni 14 za ujenzi huo lakini fedha hizo zimebaki kwenye akaunti
bila matumizi huku watendaji wakilumbana kwenye
vikao.
RC Makonda amesema
kinachomsikitisha zaidi ni kuona mshauri wa mradi amebadili mchoro wa Mwonekano
mpya wa fukwe ambao ndio ulioombewa fedha kiasi cha Bilioni 14 na kuja mchoro
wake mwingine wa Shilingi bilioni 40 bila kujua fedha hizo zitatoka wapi jambo
ambalo RC Makonda amelizungumzia kama mpango wa
hujuma kwa serikali.
Aidha RC Makonda
amewataka wananchi wajue kuwa
kinachochelewesha mradi ni uzembe unaofanywa na watendaji wachache ambao wameishia
kushinda kwenye vikao.

Post a Comment