MEYA ILALA WAUMINI WAKIWEZESHWA KIUCHUMI SADAKA MAKANISANI ZITAONGEZEKA ,AWATAKA KUOMBA MIKOPO YA HALMASHAURI.
Na John Luhende
Mwamba wa habari
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Omary
Kumbilamoto , amewataka wachungaji kuwahamasisha
waumini wa makanisa yao kujiunga katika vikundi ili waweze kupatiwa
mikopo isiyokuwa na riba inayo tolewa na Halmashauri, na kumuombea Rais
John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliongoza
taifa na kuwezesha watoto wa masikini kupata elimu bure .
Meya Kumbilamoto ametoa kauli hiyo katika
kanisa la EAGT Vingunguti alipokuwa akitoa sadaka ya shukrani
ambapo pia ametoa mifuko 20 ya saruji na mchanga roly moja
kwaajili ya kumalizia ujenzi wa kanisa hilo na kusema kuwa njia pekee ya
kuya saidia makanisa kupata sadaka nyingi ni kuwawezesha waumini kuwa na kipato.
‘’Mahali hapa
ni mahali sahini mliniombea
wakati nagombea nami niliahidi kuwa
nitamshukuru Mungu kwa kunifanikisha leo nime kuja na sadaka yangu ya
shukrani pamoja na hilo pia mmenieleza kuwa mnataka kumalizia
ujenzi wa kanisa mnahitaji mifuko 20 ya
saruji leo nina wapa mifuko 10 , niutapa
tena mingine 10 mkitumia hii ikiisha pia ntamtuma katibu atawaletea mcha lory
moja ‘’Alisema
Aidha ame mshukuru rais Magufuli kwa kutoa
elimu bure na kusema kuwa kata ya vingunguti wananchi wake wengi ni
masikini kwa kuungamkono elimu bure kwa kushirikia na na wadau
mbalimbali wamefanikiwa kuinua kiwango cha ufauli kwa wanafunzi kwa kutoa
chakula kwa shule zote za kata hiyo.
Kwaupande wake Mchungaji kiongozi wa
kanisa la EAGT upendo Vingunguti Marttini Mhokole
pamoja na kushuru meya kwa msaada huo , amewataka watu wenye
fedha kuzitazama nyumba za ibada kwani huko ndiko watu wanajengwa
kiroho na kufanya taifa kumcha Mungu.
‘’Niviongozi wachache sana wanaokumbuka baada ya
kufanikiwa tunamshukuru sana Meya kwa
msaada huu naomba na viongozi wengine tusiache ktoa kwaajili ya nyumba za ibada taifa hili linategemea kujengwa na wacha
Mungu tusiliache likaharibika kwa kutokuwa na viongozi wasiokuwa na hofu ya
Mungu’’Alisema
Wakati akitoa msaada huo alitaka
waumini wasichangishwe kwaali ya ujenzi huo kwakuwa yeye amemalizia
, waumini wa kanisa hilo wamepokeaje msaada huo wamepokea kwa shangwe
msaada huo na kusema kuwa wataelekeza nguvu zao katika kufanya mambo mengine
baada ya ujenzi huo kumalizika .

Post a Comment