Ads

SIMBA KUIFUATA VITA CLAB NCHINI CONGO


Baada ya kuanza vyema kampeni ya kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka jijini Dar es salaam Alhamisi ijayo kuelekea DR Congo tayari kwa mchezo wa raundi ya pili dhidi ya AS Vital
Mchezo huo utapigwa Jumamosi, Januari 19 mwaka huu, ambapo Simba inakwenda Congo kusaka japo alama moja katika mchezo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkali hasa ikizangiwa Vita Club ilipoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Al Ahly
Kocha Mkuu wa Simba Patrick Aussems amesema kipaumbele chao ni kushinda michezo yote ya nyumbani na kuhakikisha hawafungwi kwenye michezo ya ugenini.
Ijumaa JS Saoura ambyao ililazwa mabao 3-0 na Simba katika mchezo wa kwanza, itakuwa mwenyeji wa Al Ahly inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa kundi D linaloongozwa na Simba

No comments