Ads

MAKAMU WA RAIS AZINDUA MRADI WA KUENDELEZA UTALII UKANDA WA KUSINI (REGROW)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mradi wa kuendeleza utalii ukanda wa kusini mwa Tanzania (REGROW) ,Kihesa Kilolo mkoani Iringa.


Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan 
amesema Serikali imedhamiria kuleta mabadiliko ya dhati katika sekta ya 
utalii kwa kuhakikisha inatanua mtandao wa barabara na pia kuweka 
mikakati dhabiti ya kuviendeleza vivutio vya utalii viliovyoko kanda ya 
Kusini ili vichangie ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi. 


Makamu
wa Rais aliyasema hayo leo kwenye hafla ya uzinduzi wa mradi wa 
kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania uliofanyika Kihesa Kilolo
mkoani Iringa.Makamu wa Rais alisema Serikali imeendelea kuandaa na 
kutekeleza mipango mikakati mabali mbali kwa lengo la kuhakikisha 
shughuli za utalii zinasambaa nchi nzima . 

Makamu wa Rais 
amasema katika kuendeleza utalii kanda ya kusini, ambapo Serikali ya 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea mkopo mwenye masharti nafuu 
Dola za kimarekani milioni 150 kutoka benki ya Dunia ambapo mradi huo 
utatekelezwa kwa miaka 6 kuanzia 2017/2018. 

Mradi huo wenye 
lengo kuu la kukuza utalii na kipato kwa wananchi kwa kuboresha miundo 
mbinu, kujenga uwezo katika usimamizi wa maliasili na kuwawezesha 
wananchi wanaozunguka hifadhi kuzalisha kwa tija .

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla kabrasha lenye Andiko la mradi wa REGROW na Mikataba ya Fedha na utekelezaji wa mradi mara baada ya kuuzindua mradi huo katika eneo la Kihesa Kilolo mkoani Iringa.




No comments