Ads

SEKTA YA DAWA ZA BINADAMU NCHINI YAPATA WAWEKEZAJI

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage akijibu swali leo Bungeni mjini Dodoma



Na Jacquiline Mrisho, Dodoma.

Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji pamoja na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) wamefanikiwa kuhamasisha baadhi ya wawekezaji kuwekeza katika sekta ya dawa za binadamu na vifaa tiba ili kupunguza uagizaji wa dawa kutoka nje ya nchi.


Hayo yamesemwa leo mjini Dodoma na Waziri wa wizara hiyo, Mhe. Charles Mwijage alipokuwa akijibu swali la Mhe. Khadija Ali (Viti Maalum) aliyehitaji kufahamu mpango wa Serikali wa kutumia malighafi zilizopo kuzalisha baadhi ya dawa na vifaa tiba.

No comments