Ads

SERIKALI KUZALISHA MEGAWATI 200 UMEME UTAKANAO NA JOTO ARDHI IFIKAPO MWAKA 2025.

 
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji Joto ardhi Tanzania (TGDC) Bw. Kato Kabaka akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

.........................

Serikali ya Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania ipo katika utekelezaji wa kuzalisha megawati 200 umeme utokanao na joto ardhi ifikapo mwaka 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Kampuni ya Uendelezaji joto ardhi Tanzania (TGDC) Bw. Kato Kabaka akitoa taarifa ya mafanikio ya uendelezaji joto ardhi Tanzania katika kipindi cha miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Bw. Kabaka amesema kuwa kulingana na mpango wa Taifa wa uzalishaji umeme wa mwaka 2020 (PSMP,2020) lengo nikuzalisha megawati 200 (MWe) za umeme na megawati 500 za joto(MWt) zitokanazo na joto ardhi ifikapo mwaka 2025.

Bw. Kabaka ameeleza  mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 60 ya Uhuru ikiwemo kujenga uwezo wa ndani tokea kuundwa kwa TGDC mwaka 2013 ambapo wataalamu waliopata mafunzo wameongezeka kutoka 7 hadi 30 kwa ngazi ya diploma hadi shahada ya uzamili, taaluma ya joto ardhi ambayo utolewa nje ya nchini.

Mafanikio mengine ni upatikanaji wa vitendea kazi kwa ajili yakufanya tafiti kama MT(5), TEM(1),Radon Counter (1) na CO2 Flux (1) ambavyo vimegharimu shilingi bilioni 1.5.

Bw. Kabaka amesema mafanikio ni mengi asingeweza kuyaeleza yote miongoni mwa mafanikio hayo ni kukamilika kwa taratibu za manunuzi za mtambo wakuchoronga (Driling Rig), kuongezeka kwa ushirikiano wa wadau wanaoendeleza joto ardhi kimataifa, kujenga uelewa wa pamoja wa manufaa na fursa za joto ardhi.

Kutekeleza miradi ya kipaumbele, kuendelea kuandaa miradi mingine ya joto ardhi,kukamilisha kuchoronga visima vifupi vya utafiti, kuendeleza miradi ya matumizi ya moja kwa moja ya joto ardhi, kubuni na kuendeleza Teknolojia mpya, kujenga uwezo wa Taasisi za ndani ya nchi, Kujenga uwezo wakuchoronga visima vya joto ardhi, kushiriki katika ushindani wa fedha za uendelezaji wa joto ardhi na kufanya kazi za ushauri elekezi ndani na nje ya nchi.

Kamishina Msaidizi wa umeme kutoka Wizara ya Nishati Styden Rwebangila, amesema Tanzania ina uwezo wakuzalisha zaidi ya megawat 15,000 za joto ardhi (MWe).

“Megawati hizo ni kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya joto ardhi, mchanganyiko wa joto, maji moto na madini una matumizi mbalimbali mtambuka ya kiuchumi na kijamii”amesema.

Amesema kuwa matumizi hayo ni uchakataji viwandani, kuongeza thamani ya mazao ya kilimo,mifugo,ufagaji wa viumbe wa majini,misitu hususani kukausha mbao,kivutio na kichocheo cha utalii na tiba kwa magonjwa mbalimbali.

Amebainisha kuwa kabla ya ukoloni chemchemi za maji moto ziliendelezwa kwa ajili ya tiba, matumizi ya mifugo (magadi) ibada na kuimarisha utawala mila na utamaduni mfano Mtagata- Kagera, Ibadakuli -Shinyanga na Amboni Mkoani Tanga.

No comments