Ads

FIDES INSURANCE AGENCY YATOA SOMO ELIMU YA BIMA.

 

Mkurugenzi wa Kampuni ya Fides Insurance Agency Bw. Sayi John Daud ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Bima nchini akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

...........

Kampuni ya Fides Insurance  Agency LTD ambao ni  wauzaji wa Bima mbali mbali iliyopo Tabata Segerea jijini Dar es Salaam imesema wanananchi  wakiwa na bidii ya  kukuza uelewa juu ya bima  zinazotelewa na makampuni italeta ahuweni wakati wa majanga.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kampuni ya Fides Insurance Agency Bw. Sayi John Daud, amesema kuwa wananchi wakiwa na uelewa  itachochea kupunguza majanga.

"Kuna baadhi  hawana uelewa na bima, hivyo jamii ikiwa na uelewa zaidi itasaidia kuepukana na majanga mbali mbali zidi ya umiliki wa vyombo vyao mbalimbali,"amesema Bw. Daudi.

Bw. Daudi ni Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Bima nchini, ameeleza kuwa  jamii inatakiwa kukata bima kwa kumaanisha ili kuepukana na changamoto ikiwemo kulipwa pale nyumba yako au gari na matatizo ikiwemo ajali.

Ameeleza kuwa tayari serikali ipo katika mpango wa kuhakikisha inawafikia asilimia 80 ya watanzania kuwa na uwelewa wa bina pamoja na asilimia 50  wawe wamepata bima  hadi kufikia mwaka 2030 .

Daudi amesema kuwa  Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Nchini ( TIRA) imekuwa ikichagiza  kufikia malengo ya serikali ambayo ni muhimu kwa Mawakala , Madalali pamoja na makampuni ya Bima kuendelea kutoa elimu kwa wateja.

Almefafanua kuwa  wao kama wakala wamekuwa wakijitaidi  kila mmoja awe na kitu cha kipekee ili wanaoshindana wasiweze kushindwa  katika kutoa huduma.

No comments