MGOMBEA UDIWANI KATA YA TUNGI,NIMEFANIKIWA KUTEKELEZA MENGI
Na John Luhende
Mwamba wa Habari
Mgombea kiti Cha udiwani CCM kata ya Tungi Kigamboni Ndugu Ernest Mafimbo amewaomba wananchi wa kata ya Tungi kuchagua Chama cha Mapinduzi na kumchagua ili awezekuwa kuwaletea Maendeleo.
Amesema hayo Katika mkutano wa kampeni uliofanyika Katika eneo la mnadani Tungi akiambatana na Mgombea ubunge wa chama hicho Dkt Faustine Ndugulile ikiwa ni mwendelezo wa kampeni .
Amesema,akiwa madarakani alifanikisha kujenga ofisi za serikali za kata hiyo kwa kushirikiana na ofisi ya Mkurugenzi na Mbunge ,pia alifanikisha kujenga ofisi za Mitaa ya kata hiyo ambapo mwanzo walikuwa wakipanga .
Pia alifanikisha kujengwa vyoo vyenye thamani ya shilingi milioni 38 Katika shule ya msingi Tungi na madarasa mawili yanayoendeleakujengwa .
Kwajuhudi zake pia amesema, alipata ufadhili wa kampuni ya mafuta ya TAZAMA na kuanza kusambaza Maji kwa wananchi wa mtaa wa magogoni ,na alifanikisha kujengwa kwa barabara kiwango cha changarawe Katika eneo korofi la pale kwa masisita kuelekea soko maziwa ambapo wakati wa mvua maji yalikuwa yanajaa.
" Wananchi naomba mjue kuto fautisha chama na vyama , CCM ndiyo chama ,,,vile vingine ni vyama vya watu Chagueni CCM ,Mimi nilikuwa chama Cha upinzani nilikuwa sawa na tochi iliyo ili wekwa gunzi badala ya betery haiwezi kutoa mwanga "Alisema .
Uwezo wa kufanya kazi utatokana na maamuzi ya wananchi kwa kuchagua CCM ili kuweza kuyaendeleza mazuri ambayo imekwisha yaanzisha na kwa kata ya tungi itanufaika na mradi wa bara bara na mifereji unaotekelezwa na DMDP amabapo mwanzao haikunufaika .
Post a Comment