Ads

Mkazi wa Dar aibuka na kitita cha Milioni mia moja kutoka Gol's Sports Betting

Juma Kidoga Mkazi wa Dar es Salaam ameibuka na zawadi nono ya kitita cha
 shilingi za kitanzania Milioni Mia Moja (sh 100,000,000) kutoka na ubashiri wa matokeo wa mechi mbali mbali .

Juma ambaye asili yake ni mkoa wa Tanga anayeishi na mke wake pamoja na watoto wao wanne muuzaji wa matunda huku mkewake akitengeneza na kuuza vitafunwa aina ya sambusa amekua akishiriki matokeo ya mechi na Kampuni ya Gal Sports Betting kwa takribani miezi mitatu sasa.

Alisema kwa kupenda kwakwe mchezo wa mpira wa miguu amejikuta anaingia
katika mchezo huu wa ubashiri wa matokeo ya mechi hali iliyopelekea kuibuka na ushindi wa kitita hicho cha fedha.

Alibainisha  kuwa anafuraha kubwa kuwa mshindi wa kiwango kikubwa cha fedha
Kama hicho nakuwa ataenda luzitumia fedha hizo kuwasaidia wazazi wake Ili
kuchangia kupewa baraka zao nikiwa naanza kutagakari  ni kwanamna gani
nitazitumia.

" Ninafuraha kubwa kuwa mshindi nitatazitumia fedha zangu kuwa saidia wazazi wangu waliopo Tanga pia kwa muda mrefu nilipoteza ndoto yangu ya kujishughulisha uuzaji wa vifaa vya umeme jambo ambapo litanifanikishia kwa sasa,"alisema Juma.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Gal's Sports Betting Hakan Aric alisema walianza kufanya shughuli zao nchini tangu mwaka 2016 na wakati huu Kampuni inaongoza kwa kuwa na maduka mengi na yenye ubora wa huduma kwa wateja wao.

Alisema viwango vyao vya ubashiri ni vya hali ya huu kwa nchi nzima na wanaongeza bidhaa zaidi kwenye wasifu wao ili kuongeza burudanijambo litakalo panua wigo wa ushindi kwa wateja bila shaka wanajiandaa kuwa miongoni kwa wachache wanaotoa zawadi stahiki kwa washindi bila kuchelewa.

"Gol's Sports Betting ni Kampuni kubwa kuliko zote nchini inayokishughulisha na
 ubashiri wa matokeo ya mechi za mpira mtandaoni ikiwa imeajiri zaidi ya wafanyakazi 1000 pamoja na wanahisa na inawateja zaidi ya Milioni kumi(10,000,000) duniani kote,"alisema Hakan.

Alisema Kampuni inaleseni ya kuendesha biashara kutoka serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa muongozo wa bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania.

Gol's Sports Betting inajipambanua kuwa inaendesha shughuli zake kwa kutumia
dirisha moja ambapo mtumiaji hutumia jina moja pamoja na namba ya ufanyaji
malipo kwenye ubashiri wowote .

No comments