Ads

MCHUNGAJI KANISA LA KRISTO AIOMBA SERIKALI KUINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI.

Kanisa la Kristo imeitaka kwa serikali kuwaondoa watu waliovamia eneo wazi lililopo karibu na kanisa hilo maeneo ya Mwembe yanga, Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Wavamizi hao wameonekana wakileta usumbufu, wakati waumini wa kanisa hilo wakiwa katika ibada, kwani wamekuwa na kelele zinazotokana na wavamizi hao wakiwa katika majukumu yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mchangaji wa Kanisa la Kristo Temeke Bw. Morris Chiuyo, amesema kuwa wavamizi hao wamejenga banda katika eneo la wazi yenye namba 307/A pamoja na kuwepo kwa watu wanaofanya kazi ya kutengeneza magari kinyume na sheria.

Mchungaji Chiuyo, amesema kuwa katika eneo hilo wazi kuna Gereji, Mama ntilie, Muosha magari, Dalali wa kuuza magari pamoja na soko la ndizi.

“Watu wa gereji wanajisaidia kwenye ukuta wa kanisa na wanamwaga girisi na oil na matambala machafu kitu ambacho sio rafiki” amesema Mchungaji Chiuyo.

Ameeleza kuwa kanisani bado linayo imani kwa viongozi wa serikali katika kusimamia sheria ili haki iweze kutendeka kwa namna moja au nyengine.

Amefafanua kuwa wametoa taarifa katika mamlaka mbalimbali lakini mpaka sasa hakuna hatua ilichukuliwa.

“Viongozi wenye dhamana ya kusimamia watanzania kwenye maeneo ya haki wanapaswa kufanya hivyo ili kuleta maendeleo”

Kanisa la kristo Temeke lipo nchini mpaka sasa ni miaka 60 likifanya kazi ya kitume kwenye kiwanja namba 21,22 na 23.

No comments