Makonda apokea Msaada kutoka kwa Balozi wa UAE kusomesha watoto wa kike 100

Hussein
Ndubikile
Mwambawahabari
Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam, Paul Makonda amepokea msaada wa kuwasomesha watoto wa kike
100 waliochaguliwa kujiunga kidato cha
tano mwaka huu wanaochukua masomo ya sayansi kutoka kwa Balozi wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE),Khalifa
Abdulrahiman Almazouqi.
Wanafunzi
waliopatiwa msaada unaojumuisha ada na vifaa vya shule ni wale waliobainika
kuwa wazazi wao hawana uwezo wa kugharamia masomo.
Akizungumza
jijini humo mkuu wa mkoa huyo alisema ameamua kujitoa kwa dhati kuwasaidia
watoto wa kike wanaochukua masomo hayo kwa kukumbuka alipotoka kwani alisaidiwa
ndugu, jamaa na marafiki kufika alipo sasa.
“ Nimefika
hapa si kwa uwezo tu wa wazazi wangu
bali nlisaidiwa na ndugu na marafiki hivyo ninao wajibu kukumbuka
nilipotoka hadi nilipofika watoto mnaowaona wazazi wao hawana uwezo
kuwasomesha,” alisema Makonda.
Alibainisha
kuwa hata Rais Dkt. John Magufuli ameonyesha dhamira ya dhati ya kuwakumbuka
wanyonge kwa kutoa elimu bure kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne.
Alisisitiza
kuwa Hayati Mwalimu Nyerere katika matamko yake alishawahi kusema ukombozi wa
mnyonge unapatikana kwa kumpatia elimu hivyo hilo kauli hiyo imempa msukumo wa
kuwasaidia watoto hao watimize ndoto zao.
Alifafanua
kuwa watoto wa kike wakipatiwa elimu
wanapata heshima kwenye jamii kwani wanakuwa na uwezo wa kuchanganua mambo na
kuchangia mambo katika ngazi ya familia.
Pia alisema
ameonelea kuanza safari ya kuwasaidia watoto wa kike kwa kuangalia kigezo cha
mazingira magumu na vishawishi wanavyokutana navyo na ugumu wa masomo hayo.
Vigezo
vingine ni umuhimu wa sayansi wakati nchi ikielekea uchumi wa kati kupitia
viwanda, kuzitafutia ufumbuzi wa wataalamu sekta ya madini na nishati pamoja na
umuhimu wa kutengeneza wanasayani wengi wa kike nchini.
Aliwahimiza
kuzingatia masomo yao ili weweze kulinda na kutimiza ndoto zao waje kulitumikia
taifa katika miaka ya baadaye na kumshukuru balozi wa UAE.
Kwa upande
wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Hamis Lisu alisema msaada uliotolewa
umewalenga watoto wa kike wenye wazazi wasiomudu gharama za masomo.
Alimshukuru
na kumpongeza Makonda kwa mchango wake katika elimu kwani ameweza kufanikisha
ujenzi wa ofisi 46 za walimu za kisasa lengo likiwa kufikisha 402 kwa michango
ya wahisani.
Lisu alisema
mkuu wa mkoa huyo ameshawasaidia walimu 800 kukopeshwa viwanja vya gharama
nafuu huku akimpongeza kuweka utaratibu mzuri wa kuwasomesha watoto hao.
Naye Balozi
wa UAE, Khalifa alisema ameamua kutoa msaada huo kwa kuwa elimu ni ufunguo wa
maisha na kuwataka watoto hao kushikilia masomo watimize ndoto zao.
Alisema
mradi huo ni wa mwanzoni na kwamba mbeleni watatoa msaada wa chakula
kufanikisha masomo yao na kumshukuru Rais Magufuli kwa sera yake ya elimu bure.
Mzazi Anna Fundi
alimshururu Makonda kwa kusaidia watoto hao kuweza kuendelea na masomo yao na
kuwataka wazazi wenzange kumuombea ili aendelee kuwa na moyo wa kusaidia.
Aliwasihi
watanzania waache kubaguana badala yake wapendane kufanikisha Tanzania kuwa
nchi iliyoendelea.
Mwanafunzi
wa Kidato cha Tano wa Shule ya Sekondari Kisutu, Velaria Reuben alimshukuru
Makonda kwa kuguswa na hali zao na kuahidi kutomwangusha katika masomo yao ili
baadae waweze kusaidia wenzao wenye uhitaji.
Post a Comment