Ads

UWT ILALA YATOA MSAADA NA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA MAMA NA MTOTO CHANIKA.



Na John Luhende  
Mwamba wa habari
Katika kuelekea  maadhimisho ya siku ya wanawake duniani , Umoja wa Wanawake wa Chama chaMapinduzi   (UWT)  Wilaya ya Ilala wameendelea kufanya kazi za kujitolea katika jamii na kutoa misaada ya kibinadamu  katika maeneo mbalimbali ambapo leo wamefanya kazi hizo katika hospitali ya Mama na mtoto chanika.


Akizungumza Hospitalini hapo mara baada ya wanawake hao kufanya kazi ya usafi na kutoa msaada katika wodi za wazazi , mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Ilala Amina Dodi , amewataka wanawake kutojiweka nyuma katika shughuli za maendeo na kugombea Nafasi  mbalimbali za uongozi badala ya kuwaachia wanaume  pekee  .

‘’Dodi amesema ,wanawake  wana wajibu wa kugombea nyazifa zozote  za uongozi zinapotangazwa wawe mstari wa mbeĺe katika kugombea wasiwe nyuma’’amesema

"Wanawake wa Wilaya ya Ilala leo tumeungana na wanawake  wote  katika siku hii ya wiki ya Wanawake wa CCM  kuanzia O ktoba Mosi hadi Octobar 3 tukishiriki usafi na kazi za kijamii" amesema. 

Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya utekelezaji  UWT  Wilaya ya Ilala  Batuli Mbaraka  Mziya, ameipongeza Serikali kwa kuwajali wanawake na kuwajengea hospital ya Mama na mtoto, na kuwataka wanawake wanapo adhimisha sikuhiyo kupendana na kusaidiana.

‘’ Naipongeza Serikaĺi ya awamu ya tano na  Rais John Magufuli kwa kujenga hospitali ya Mama na Mtoto  hapa  kata ya Chanika ni jambo jema wanawake kwa sasa wanajifungua  karibu na eneo lao hawasumbuki tena kufuata huduma hizi  Amana” amesema

Naye Diwani wa Viti Maalumu  Wanawake Manispaa ya Ilala Neema Nyangarilo, aliwataka wanawake wa Wilaya ya Ilala kuchangamkia fursa za  kiuchumi  na mikopo inayotolewa na serikali ili kujiendeleza kibiashara na kuinua kipato chao .

Kanansia Michael  Shoo , ni Daktari kiongozi wa Hospitali hiyo akitoa neno la shukrani amewashukuru  wanake wa  UWT Ilala kwa moyo wao wa kujali na kuyataka makundi mengine kuwa na moyo huo.
Siku ya wanawake duniani kwa wana ccm , huadhimishwa kila mwaka ifikakapopo  tarehe Mosi  hadi 3 Oktoba , ambapo wanakewa huzitumia siku hizo kufanya shughuli za kujitolea katika jamii.











No comments