Ads

CRDB yataja washindi wawili wa wiki wa Shindano la Shinda na SimAccount




Na.Hussein Ndubikile, 
Mwambawahabari
Washindi wawili wamejipatia kitita cha Sh.Mil 3 kupitia Shindano la Shinda na  SimAccount linaloendeshwa na Benki ya CRDB ambapo benki hiyo huchezesha droo ya shindano hilo na kuwataja washindi.

 Akichezesha droo hiyo mbele ya wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Meneja Masoko wa benki hiyo, Ariel Mkony alimtangaza mshindi wa kwanza aliyepatikana kutoka mkoani Lindi aliyejitambulisha kwa jina la Cuthbert Mwakatumbula(34) ambaye pia ni askari Magereza aliyeshinda fedha taslimu Sh.Mil 2.
Amesema tangu waanze kuchezesha shindano hilo wamekuwa na utaratibu wa kuwataja washindi wa wiki na mwezi ambapo hujinyakulia fedha taslimu kwa kujisajili katika huduma ya SimAccount.
“Shindano linaendelea vizuri tunawaomba wananchi waendelee kucheza kwa kujiunga na huduma ya SimAccount  itayowafanya wateja wajikwamue kiuchumi,”amesema Ariel.
Kwa upande wake,Mshindi, Cuthbert amesema amepokea kwa furaha zawadi hiyo na kwamba imemuaminisha kuwa shindano hilo halina upendeleo.
Naye, Adela Kaliseni (40) mshindi kutoka wilayani Korogwe, Tanga amepokea taarifa ya ushindi wa kitita cha Sh. Mil 1 huku haamini na kusisitiza ataamini mpaka atapoingiziwa fedha zake kwenye akaunti yake.
Kaliseni ambaye ni Askari Magereza mkoani humo amebainisha fedha hizo atazitumia kuongeza ng’ombe wa kisasa wa maziwa.
Benki yaCRDB kupitia Meneja huyo imesema mpaka jumla ya washindi 684 wamejishindia fedha taslimu tangu kuanzishwa kwa shindano hilo huku washindi 648 wakijishindia fedha taslimu Sh 5,000, Sh 20,000  katika nyakati za asubuhi na jioni .
Ameongeza kuwa hadi sasa washindi wa kila wiki 36 wamejishindia fedha taslimu  Sh mil 2 na Sh Mil 1 na Kubainisha wiki ijayo watachezesha droo ya mwezi ya Sh Mil.10.
“ Mteja hana haja kwenda kwenye tawi la benki au wakala kupanga foleni bali anaweza kujiunga kupitia simu ya mkononi kwa kupiga *150*62 # , akiwa na kitambulisho cha kupigia kura anaingiza namba zilizomo kwenye kitambulisho’” amesema.
Balozi wa SimAccount, Zena Mohamed ‘Shilole’ amewataka wananchi kushiriki shindano hilo kwani litawasiadia kujikwamua kiuchumi.

No comments